Subscribe:

Pages

Featured Posts

JK AZINDUA BENKI YA FIRST NATIONAL BANK OF TANZANIA

A round of applause rings after President Jakaya Mrisho Kikwete has officially launched the First National Bank Tanzania (FNB-Tanzania) yesterday at the Kilimanjaro Grand Hyatt hotel in Dar es salaam. Others from left are the High Commissioner of South Africa to Tanzania, Mr Thanduyise Henry Chiliza, the CEO of First Rand, Mr Sizwe Nxasana and the Deputy Permanent Secretary in the Ministry of Finance Ms Elizabeth Nyambibo.
President Jakaya Mrisho Kikwete makes his keynote speech during the official launch of  the First National Bank Tanzania (FNB-Tanzania) yesterday at the Kilimanjaro Grand Hyatt hotel in Dar es salaam today February 2, 2012

JESHI LINALOTAWALA NCHINI MISRI LATANGAZA SIKU TATU ZA MAOMBOLEZO

Jeshi linalotawala nchini Misri  latangaza siku tatu za maombolezo ya watu zaidi ya watu 70  wamefariki kufuatia ghasia kati ya mashabiki wa timu mbili katika mji wa Port Said, nchini Misri.

Taarifa hizo ni kwa mujibu wa televisheni ya taifa ya MISRI ambayo imeeleza kuwa Watu hao walikufa baada ya mashabiki kuanza kuingia uwanjani, baada ya mechi kati ya vilabu viwili vikuu vinavyoongoza ligi nchini humo, Masry na Al-Ahly, siku ya Jumatano.

Inahofiwa kwamba idadi ya vifo huenda ikaongezeka, kwani zaidi ya watu 156 wamejeruhiwa kati ya waliokufa ni pamoja na maafisa wa usalama.
Ukosefu wa usalama mkali ambao hudumishwa kwa kawaida huenda ikawa ni jambo ambalo lilichangia kutokea ghasia hizo.

Polisi nchini Misri wametulia mno tangu kufanyika maandamano yaliyomtoa Rais Hosni Mubarak madarakani.
Katika mechi hiyo ya Jumatano, timu ya Port Said, Masry, ilipata ushindi wa magoli 3-1.

Walioshuhudia walielezea kwamba kulikuwa na hali ya wasiwasi muda wote wa mechi hiyo, tangu shabiki mmoja wa Al-Ahly alipoinua bango ambalo inadaiwa lilikuwa linawatukana mashabiki wa timu ya nyumbani.

Maafisa wachache wa polisi walijitahidi kuwapa ulinzi wachezaji, lakini hawakufanikiwa kabisa na Sehemu moja ya uwanja ilichomwa moto.

Maafisa wanaohusika wameelezea kwamba vifo vingi vilitokana na watu kupata majeraha makubwa ya kichwa kwa kupigwa au kukatwa, na wengine kuzimia hadi kufa wakati wa mkanyagano.

Mechi zote za ligi kuu zimefutiliwa mbali, na bunge jipya la Misri linakutana leo  katika kikao cha dharura kuujadili msiba huu.

SHYROSE BHANJI KALAZWA MAUTUTI

Afisa uhusiano wa NMB na aliyekuwa mgombea nafasi ya kuwa mwakilishi wa Ubunge Kinondoni kupitia chama cha Mapinduzi Dada Shyrose Bhanji akiwa amelazwa.
Hii ni kutokana na hali yake ya kiafya kuwa mbaya sana,mungu msaidie binti yetu Shyrose.

MAKAMU WA RAIS DKT BILAL AWEKA JIWE LA MSINGI MRADI WA UJENZI WA KITUO CHA MNADA WA NG’OMBE KIJIJI CHA MKIU, AWEKA JIWE LA MSINGI MRADI WA SHAMBA LA KUKU.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akipanda mti wa kumbukumbu katika eneo la mradi wa Ujenzi wa Kituo cha mnada wa Ng’ombe katika Kijiji cha Mkiu Wilaya ya Mkuranga, wakati akiwa katika ziara yake ya Mkoa wa Pwani leo, Januari 02, 2012. 
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiweka Jiwe la Msingi la mradi wa ujenzi wa Kituo cha mnada wa Ng’ombe katika Kijiji cha Mkiu Wilaya ya Mkuranga,  akiwa katika ziara yake ya Mkoa wa Pwani, leo Januari 02, 2012.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akitembelea na kukagua mradi wa ujenzi wa Kituo cha mnada wa Ng’ombe katika Kijiji cha Mkiu Wilaya ya Mkuranga, akiwa katika ziara yake ya Mkoa wa Pwani, leo januari 02, 2012.

 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiweka Jiwe la Msingi katika Kituo cha Mradi wa shamba la Kuku lililopo Kijiji cha Mkiu, Wilaya ya Mkuranga, mkoa wa Pwani, linalomilikiwa na Mtanzania mzawa, Abdulwahd Mohamed (kulia), wakatia akiwa katika ziara yake ya Mkoa wa Pwani leo Januari 02, 2012.
 Makamu wa rais wa Jamhuri ya Muugano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisikiliza maelezo kutoka kwa mtaalum, kuhusu ufugaji wa Kuku wa mayai, wakati alipotembelea na kuweka Jiwe la msingi katika kituo cha Shamba la Kuku kilichopo Kijiji cha Mkiu Wilaya ya Mkuranga, Mkoa wa Pwani, leo Januari 02, 2012, wakati akiwa katika ziara yake ya Mkoa wa Pwani.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akitembelea na kukagua mabanda ya kufugia kuku katika kituo hicho cha Shamba la Kuku kilichopo Kijiji cha Mkiu Wilaya ya Mkuranga akiwa katika ziara yake ya Mkoa wa Pwani, leo Januari 02, 2012.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, akitembelea na kukagua mabanda ya kuku katika kituo cha Shamba la Kuku kilichopo Kijiji cha Mkiu Wilaya ya Mkuranga Mkoa wa Pwani, wakati akiwa katika ziara yake ya Mkoa wa Pwani leo Januari 02, 2012. Kushoto ni Mkurugenzi wa kituo hicho, Abdulwahd Mohamed na (kulia) ni Mama Zakhia Bilal.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akipanda mti wa kumbukumbu nje ya Kituo cha Shamba la Kuku cha Kijiji cha Mkiu, baada ya kuweka jiwe la msingi na kukagua kituo hicho kilichopo Wilaya ya Mkuranga Mkoa wa Pwani, wakati akiwa katika ziara yake ya Mkoa wa Pwani leo, Januari 02, 2012. 

SIMBA YAICHAPA JKT OLJORON

Club ya simba imeibuka na ushindi wa mabao mawili kwa bila dhidi ya timu ya JKT Oljoro katika mchezo uliofanyika uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam mabao hayo yalifungwa na mchezaji wa simba Emanuel Okwi.
Simba walicheza pungufu baada ya mchezaji Haruna Moshi kutolewa nnje kwa kadi nyekundu.

FRANCIS CHEKA MADA MAUGO KUGOMBEA UBINGWA WA IBF RAUNDI 12 APRIL 28 PTA SABASABA


Bondia Fransic Cheka akizungumza na waandishi wa habari leo kupigania ubingwa  IBF raundi 12 litakarofanyika katika ukumbi wa PTA Sabasaba Aprili 28
Bondia Mada Maugo akiongea na waandishi wa habari wakati wa kusaini mkataba uho leokupigania ubingwa  IBF raundi 12 litakarofanyika katika ukumbi wa PTA Sabasaba Aprili 28.

Makamu mwenyekiti wa Oganaizesheni ya ngumi za Kulipwa Nchini, Madaraka Nyerer (Kushoto) akiwaelekeza mabondia Fransc Cheka kulia na Mada Maugo jinsi ya kusaini mkataba wa makubaliano wa kupigania ubingwa  IBF raundi 12 litakarofanyika katika ukumbi wa PTA Sabasaba Aprili 28

JK AKUTANA NA RAIS WA MAHAKAMA YA HAKI ZA ZA BINADAMU, AREJEA DAR JUMANNE USIKU

RAis Jakaya Mrisho Kikwete akipokewa na Makamu wa Kwanza wa Rais Dr Mohamed Gharib Bilali na Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Bw Saidi Meck Sadiki

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimsindikiza Rais wa Mahakama ya Haki za Binadamu ya Afrika Jaji Gerald Miyungeko,  aliyemtembelea jana baada ya kikao cha 18 cha Umoja wa Afrika jijini Addis Ababa, Ethiopia.

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiongea na Rais wa Mahakama ya Haki za Binadamu ya Afrika Jaji Gerald Miyungeko aliyemtembelea jana baada ya kikao cha 18 cha Umoja wa Afrika jijini Addis Ababa, Ethiopia.wengine ni Makamu wa Rais wa Mahakama hiyo Jaji  Sophia Akufo  (wa pili kulia) na Jaji  Nwanuri.

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AANZA ZIARA YAKE YA MKOA WA PWANI WILAYANI RUFIJI KWA KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akifurahia ngoma ya asli ya kabila la Kisukuma, wakati wa makaribisho yake alipowasili mji mdogo wa Utete Makao Makuu ya Wilaya ya Rufiji kwa ajili ya kuanza ziara yake ya Mkoa wa Pwani leo Januari 01, 2012.


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiweka Jiwe la Msingi wakati alipofika kukagua mradi wa ujenzi wa nyumba 14 za Watumishi eneo la Lugongwe, Utete Wilaya ya Rufiji leo Januari 01, 2012, alipoanza ziara yake ya Mkoa wa Pwani. Kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mwantum Mahiza.


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akitembelea na kukagua mradi wa ujenzi wa Nyumba 14 za watumishi, zinazoendelea kujengwa eneo la Lugongwe, Utete Wilaya ya Rufiji, akiwa katika ziara yake ya Mkoa wa Pwani leo Januari 01, 2012.

WAZIRI MKUU AKIZUNGUMZA NA MWENYEKITI WA TUME YA TAIFA OFISINI KWAKE BUNGENI

Waziri Mkuu, Mizengo pinda akizungumza na Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji Mstaafu. Damian Lubuva  (watatu kushoto) , makamu Mwenyekiti wa Tume,  Mh. Hamid M  Hamid na Mkurugenzi wa Tume ya  Uchaguzi, Julius Mallaba. Mazungumzo hayo yalifanyika ofisini kwake Bungeni Mjini Dodoma Februari 1, 2012.

AIRTEL MZUKA DROO MHUDUMU WA STATIONARI AIBUKA MSHINDI WA MLIONI 50 YA AIRTEL

Mhuduma wa Stationari Magomeni aibuka mshindi wa mlioni 50 ya Airtel MZUKA
Mshindi wa pili wa million 50 katika promosheni ya Mzuka wa Airtel apatikana.
Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel Tanzania Jana iliendesha draw
kubwa ya pili ya kutafuta mshindi wa milioni 50/TZS iliyofanyika jana
usiku Majira ya saa mija na nusu na kurushwa live katika kituo cha
television cha ITV na kushuhudiwa na watanzania wengi ambapo Bi Halima
Omary Issa mkazi wa Magomeni Makanya aliibuka  mshindi wa kitita hicho
cha shilling million 50 pesa tasilimu.
Bi Halima Omary mwenye umri wa miaka 26 aliyeajiriwa kama mfanyakazi
wa stationary alisikika kuwa mwenye furaha iliyozidi kifani pale
alipopigiwa simu na Meneja uhusiano wa kampuni ya Airtel Bw Jackson
Mmbando na kupewa habari njema ya kuwa mshindi wa pili wa droo kubwa
na kujishindia million 50 pesa taslimu.
Katika maojiano na mshindi huyo yaliyofanyika kupitia televisheni ya
ITV live bi Halima Omari alisikika akisema “namshukuru sana mungu yani
sewezi kuamini nilishiki sana promosheni hii na nashukuru sana kuibuka
mshindi katika promosheni ya hii ya Airtel”
Akiongea kwa niaba ya kampuni ya simu za mkononi ya Airtel meneja
Uhusiano wa Airtel Jackson Mmbando “kupitia promosheni hii kabambe
tayari tumempata mshindi wetu wa droo kubwa yapili ya milioni 50 TZS
ya MZUKA lakini bado tumebaki na zawadi nyingi za simu mpya za kisasa
za sumsung tablet pamoja na muda wa maongezi na pia  mwisho wa mwezi
wa pili tutampata mshindi wa droo ya tatu wa milioni 50/-TZS ya
promosheni hii ya MZUKA”
Pia alitumia nafasi hiyo kuwashukuru watanzania na wateja wa Airtel
kwa kuendelea kutumia huduma za Airtel na kushiriki katika promosheni
hiyo,
Promosheni ya Mzuka inaendeshwa na Airtel kwa kipindi cha miezi mitatu
mfululizo ambapo ilizinduliwa rasmi mwishoni mwa mawka jana desemba
hadi mwishoni mwa februari mwaka huu 2012.
Zawadi kabambe wanazojishindia wateja kila siku ni pamoja na simu aina
ya Samsung, Muda wa maongezi, wakati washindi wa wiki wanajishindia
Samsung ipad, na washindi wa kila mwenzi pesa taslimu shilling million
50
Promosheni ya mzuka wa Airtel bado inaendelea hadi mwisho wa mwenzi wa
februari ambapo  zawadi mbalimbali zinaendelea kutolea na droo kubwa
ya mshindi wa tatu itachezeshwa mwishoni mwa mwenzi huu.
Kujiunga ni bure tuma ujumbe wenye neno “Mzuka” kwenda namba “15565”
na ujipatie nafasi ya kuibuka kuwa moja kati ya washindi.

USIKU MAALU WA AIRTEL NA WATEJA WAKE MWANZA KATIKA UKUMBI WA GOLD CREST HOTEL.

Afisa Mauzo wa Airtel Kanda ya Ziwa Violet Gyumi akimkabidhi zawadi ya modem na kifurushi cha kuanzia kwa Subira S. Ally mara baada ya bahati nasibu kufanyika katika usiku maalu wa Airtel na wateja wake Mwanza katika ukumbi wa Gold Crest Hotel.
Wateja wa Airtel mara baada ya kupokea zawadi zao wakati walipohudhuria hafla ya kufungua mwaka iliyoandaliwa kwaajili ya wateja wa  Airtel Mwanza na kufanyika katika Hotel ya Gold Crest
Afisa uhusiano Airtel Kanda ya Ziwa Violet Gyumi akimkabidhi zawadi Mkurugenzi wa kampuni ya Barmedas Hirnoy Barmedas katika halfa iliyofanyika kwaajili ya kuwashukuru wateja wa Airtel mkoani mwanza katika hotel ya Gold Crest nakuhudhuriwa na wadau mbalimbali.

WAZIRI MKUU AKIWA KATIKA VIWANJA VYA BUNGE

 Waziri Mkuu,Mizengo  Pinda akizungumza na Mbunge wa Busega, Titus Kamani kwenye viwanja vya Bunge Mjini Dodoma Januari 31, 2012.

Waziri Mkuu, Mizengo  Pinda akifurahia jambo katika mazungumzo kati yake na Mbunge  wa Mkuranga na Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Adam Malima (watatu kulia), Mbunge wa Kigoma Kusini David  Kafulila  (wapili kulia)  na Mbunge wa Gairo Ahmed Shabiby.
Waziri   Mkuu, Mizengo Pinda akizungumza na Mbunge wa Kigoma Kusini, David Kafulila kwenye viwanja vya Bunge Mjini Dodoma Januari 31, 2012.

BASATA, JESHI LA POLISI WAUNDA KIKOSIKAZI KUDHIBITI UHARAMIA KWENYE SANAA

Kaimu Katibu Mtendaji wa BASATA, Godfrey Lebejo akisisitiza jambo kwenye programu ya Jukwaa la Sanaa inayofanyika kila wiki makao makuu ya Baraza hilo Ilala Sharif Shamba na kuhudhuriwa na wadau wa Sanaa. Kulia kwake ni Afisa Uhusiano wa Uhamiaji Bi. Tatu Burhan.
Ssp Edson Kasekwa kutoka Jeshi la Polisi Makao Makuu, Kitengo maalum cha Operesheni uzuiaji uhalifu akitoa ufafanuzi wa masuala mbalimbali kuhusu matumizi ya Sanaa katika Polisi Jamii na Ulinzi Shirikishi. Kulia kwake ni Mkurugenzi wa Ukuzaji Sanaa, BASATA Bi. Vivian Shalua.

Afisa Uhusiano wa Idara ya Uhamiaji Tatu Burhan akieleza haja ya Jamii kushirkiana na Idara yake katika kupambana na tatizo la Uhamiaji haramu nchini. Kushoto kwake ni Bw. Lebejo.
Kikundi cha Ngoma cha Jeshi la Polisi kikitumbuiza kwenye Programu ya Jukwaa la Sanaa ambapo elimu kuhusu dhana ya Ulinzi Shirikishi na Polisi Jamii ilitolewa kwa Wadau zaidi ya 140.
Sehemu ya Maafisa wa Jeshi la Polisi wakifuatilia matukio mbalimbali kwenye Programu hiyo ya Jukwaa la Sanaa.
Mkongwe wa Sanaa za Maonyesho Mzee Nkwama Bhallanga akielezea masuala mbalimbali kuhusu Sanaa Shirikishi katika Polisi Jamii na Ulinzi Shirikishi.
Wadau wa Sanaa wakiifuatilia Programu ya Jukwaa la Sanaa wiki hii.

Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) na Jeshi la Polisi nchini wameunda kikosikazi maalum kitakachokuwa kikifuatilia uharamia na maovu mbalimbali katika shughuli za Sanaa na Burudani.

Kikosikazi hicho kimeundwa baada ya Jeshi la Polisi nchini kutumia Sanaa shirikishi katika kutoa elimu kwa wadau wa Sanaa kuhusu dhana ya polisi jamii na ulinzi shirikishi kwenye Jukwaa la Sanaa linalofanyika kila wiki makao makuu ya BASATA Ilala Sharif Shamba.

Akizungumza kuhusu kikosikazi hicho, Mkurugenzi wa Ukuzaji Sanaa, BASATA Bi. Vivian Shalua alisema kuwa, kazi kubwa ya kikosi hiki itakuwa ni kufuatilia maonesho yasiyokuwa na vibali, uharamia kwenye kazi za wasanii na wasanii kutoka nje wanaoingia nchini kinyume cha sheria.

Aliyataja majukumu mengine ya kikosikazi hicho kuwa ni pamoja na kudhibiti maonesho yanayodhalilisha utu na maadili ya mtanzania, kusimamia utoaji vibali kwa wasanii wa kitanzania wanaoenda kufanya maonesho nje ya nchi na majukumu mengine yatakayojitokeza.

“Kikosikazi hiki kitakuwa tayari kufuatilia taarifa yoyote ya uharamia kwenye kazi za wasanii, maonesho yanayodhalilisha utu na maadili ya mtanzania na wasanii wanaoingia ndani ya nchi na kufanya maonesho bila vibali” alisisitiza Shalua.

Kikosikazi hicho kinaundwa na Shani Kitogo (Afisa Utamaduni Ilala), Tatia Ramadhan (Polisi, TAZARA), Afande Jeremiah (Polisi Kati), Koplo Juma Mashauri (Polisi Airport), Michael Kagondela (Idara ya Utamaduni), Afande Deus Matoro (Reli) na Afande Swai (Traffic),
Wengine ni Vivian Shalua (BASATA), Jonathan Abel na Tatu Burhan (Uhamiaji), Deus Kessy (Polisi Reli), Koplo Josephat Syllively (Polisi – Maji), Masanja Nyalali (Polisi – Airport) na PC Mwakajaby (Polisi – TAZARA)

Akizungumza kwenye Jukwaa hilo la Sanaa, Asp Edson Kasekwa kutoka Polisi Makao Makuu Kitengo maalum cha Operesheni uzuiaji uhalifu,alisema kuwa, Jeshi la Polisi linawategemea wadau wa Sanaa wakiwemo wasanii katika kutoa taarifa juu ya matukio ya uharamia na uhalifu kwa ajili ya ufuatiliaji na udhibiti.

“Ni vema Wasanii na wadau wa Sanaa kwa ujumla wakaonesha ushirikiano kwa Jeshi la Polisi katika kutoa taarifa na kudhibiti uharamia na maovu kupitia sekta ya Sanaa. Hii ndiyo maana ya dhana hii ya polisi jamii na ulinzi shirikishi ya polisi kushirikiana na jamii” alisema Afande Kasekwa.

Kikosikazi hiki kimeundwa huku kukiwa na taarifa za uwepo wa vikundi mbalimbali vinavyofanya maonesho yenye kudhalilisha utu na maadili ya mtanzania huku uharamia kwenye kazi za Sanaa ukizidi kushika kasi.

WANAOTEMBELEA KWA SIKU