Shirikisho
 la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) linaipongeza klabu ya Azam kwa ushindi
 wa mabao 2-1 ilioupata timu yake katika mechi ya raundi ya kwanza ya 
michuano ya Kombe la Shirikisho.
Mechi
 hiyo dhidi ya Barrack Young Controllers II ilichezwa jana jijini 
Monrovia, na timu hizo zitarudiana wikiendi ya Aprili 6 au 7 mwaka huu 
kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. 
Ushindi
 huo unaiweka Azam chini ya kocha wake Stewart John Hall katika 
mazingira mazuri ya kusonga mbele baada ya mechi ya marudiano. Bila 
shaka ushindi wa timu ya Azam pamoja na mambo mengine umechangiwa na 
klabu hiyo kujipanga vizuri.
Hata
 hivyo ushindi huo bado ni changamoto kwa wachezaji, benchi la ufundi na
 uongozi wa Azam kuhakikisha unajipanga vizuri kwa mechi ya marudiano 
kwa vile mpira wa miguu una matokeo ya aina tatu; kushinda, kutoka sare 
au kufungwa.
Msafara
 wa timu ya Azam unaoongozwa na mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya TFF, 
Blassy Kiondo unatarajiwa kurejea nchini kesho alfajiri kwa ndege ya 
Kenya Airways kupitia Nairobi.




0 maoni:
Post a Comment