Monday, September 2, 2013

NBC YAFANYA PATI

 Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya  NBC Tanzania, Mizinga Melu akizungumza katika hafla iliyoandaliwa na benki hiyo baada ya uzinduzi wa kitengo cha Huduma Binafsi za Kibenki kwa Wateja Wakubwa cha NBC jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki. Kitengo hicho kipo katika Jengo la Coco Plaza karibu ya ufukwe  wa Coco Beach jijini humo
 Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Harry Kitillya
> (kulia) akisalimiana na Meneja wa Tawi la NBC Sea Cliff, Mariam Kombo
> katika hafla hiyo jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki. Katikati  ni
> Mkurugenzi Mtendaji wa NBC, Mizinga Melu
 Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Harry Kitillya
> (kulia) akisalimiana na Mkuu wa Idara Huduma za Kibenki kwa Wateja
> Wakubwa na Uwekezaji  wa Benki ya NBC, Andre Potgieter katika hafla
> iliyoandaliwa na benki hiyo baada ya uzinduzi wa kitengo cha Huduma
> Binafsi za Kibenki kwa Wateja Wakubwa jijini Dar es salaam mwishoni
> mwa wiki. Kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa NBC, Mizinga Melu na wa
> pili kulia ni mteja wa benki hiyo, Paul Chizi
 Mkuu wa Kitengo cha Huduma Binafsi za Kibenki kwa Wateja Wakubwa
> cha NBC, Andrew Massawe akizungumza katika hafla hiyo. Pamoja naye ni
> baadhi ya maofisa katika kitengo hicho cha wateja binafsi wakubwa.
>
 Ofisa Mwendeshaji  Mkuu wa Benki ya NBC, Maharage Chande (kushoto)
> akisalimiana na mmoja wa wateja wa benki hiyo, Paul Chizi katika hafla
> hiyo. Wengine katikati ni  Mkuu wa Idara Huduma za Kibenki kwa Wateja
> Wakubwa na Uwekezaji  wa Benki ya NBC, Andre Potgieter na Kamishna
> Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Harry Kitillya
 Mmoja wa wateja wa NBC, Paul Chizi akiipongeza Benki ya NBC kwa
> jitihada za kuanzisha kitengo maalumu cha kuhudumia wateja wakubwa
> (Private Banking).
Wasanii wa kikundi cha sarakasi cha  Mama Afrika wakitoa burudani
> katika hafla hiyo

0 maoni:

Post a Comment

WANAOTEMBELEA KWA SIKU