Thursday, April 14, 2011

MISS UTALII NAMBA MOJA HADI TATU KUANZA MASOMO LEO

Ikiwa ni sehemu ya zawadi za washindi 1-3 wa Miss Utalii Tanzania 2010/2011,Adelqueen Jonzi (mshindi wa 1),Happywitney Andrew (mshindi wa pili) na Mariam Rabii (mshindi wa tatu),wataanza masomo ya diplom katika chuo cha Dar es Salaam City Collagekilichopo nje kidogo ya jiji la Dar Es Salaam maeneo ya kimara kirungure.

Washindi hao tayari walisha kabidhiwa fomu za kujiunga na chuo hicho,ambacho kilidhamini fainali za Taifa za Miss Utalii Tanzania 2010/2011.Wataanza rasmi masomo yao tarehe 14-4-2011.Mshindi wa kwanza atasomea diploma ya Journalism and Mass communication,mshindi wa pili  atasomea diploma in Human Resouces management na Public Relations na mshindi wa tatu atasomea diploma in Business administration.
 
Tunawashukuru sana chuo cha Dar Es Salaam  City Collage,kwa kutoa nafasi hizo za elimu kwa warembo hawa,tunaamini hii ni zaidi ya zawadi kwa washindi kwani elimu watakayoipata chuoni hapo itawanufaisha wao,taifa,familia zao na hata sekta nzima ya urembo wa kitalii.Wito wetu kwa warembo hawa ni kwamba wasome kwa bidii na wazingatie masomo,kwani hii ni fulsa adimu na ya pekee kwao,ambayo wakiitumia vyema itakuwa ni ufunguo wa maisha yao ya sasa na badae.

 katika miss utalii tanzania organisation,tumefarijika na hatua ya warembo hawa kuanza masomo,ikiwa ni kuonyesha umakini na uhakika wa utekelezaji wa ahadi tulizotoa kwa washiriki na washindi.

0 maoni:

Post a Comment

WANAOTEMBELEA KWA SIKU