Friday, January 27, 2012

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL ATEMBELEA MASHAMBA YA MPUNGA YA KOROGWE, AWEKA JIWE LA MSINGI JENGO LA UKUMBI NA OFISI YA HALMASHAURI YA KOROGWE

Makamu Wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisalimiana na Madiwani wa Kata za Wilayani Korogwe, alipowasili eneo hilo kwa ajili ya kuweka Jiwe la Msingi katika Jengo la Ukumbi na Ofisi ya Halmashauri ya Wilaya ya Korogwe, wakati akiwa katika ziara yake ya Wilaya ya Korogwe mkoa wa Tanga jana, Januari 27, 2012. 

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiweka Jiwe la Msingi katika jengo jipya la Ukumbi na Ofisi ya Halmashauri ya Wilaya ya Korogwe, wakati alipokuwa katika ziara yake ya kukagua miradi ya maendeleo ya Wilaya ya Korogwe mkoa wa Tanga jana Januari 26, 2012.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal na Viongozi wa Wilaya ya Korogwe, wakikagua jengo la Ukumbi na Ofisi ya Halmashauri ya Korogwe baada ya kuweka jiwe la Msingi katika jengo hilo alipokuwa kwenye ziara yake ya kukagua miradi ya maendeleo ya wilaya hiyo jana Januari, 26, 2012. 

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisikiliza maelezo kutoka kwa mmoja wa wakulima wa Mpunga kuhusu kilimo hicho cha umwagiliaji wakati alipotembelea na kukagua mashamba ya Skim Mamlaka ya mji wa Mombo jana Januari 26, 2012.

:- Makamu wa Rais wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohamed Gharib Bilal, akikagua mitaro ya maji yanayotumika kumwagilia mashamba ya mpunga ya Skim, mji wa Mombo, wakati akiwa katika ziara yake ya kukagua miradi ya maendeleo ya Wilaya ya Korogwe mkoa wa Tanga jana Januari, 26, 2012, akiwa katika ziara ya mkoa wa Tanga. 
:- Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisoma ujumbe ulioandikwa na vijana wa Harakati ya Mazingira, wakati akiwasili kwenye uwanja wa Mamlaka ya Mji wa Mombo kwa ajili ya kuwahutubia wananchi, akiwa katika ziara yake ya Wilaya ya Korogwe Mkoa wa Tanga, jana Januari26, 2012. Kulia kwake ni mkewe Mama Zakhia Bilal na (kushoto) ni Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Chiku Galawa.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akimkabidhi Kombe, Kiongozi wa timu ya Mombo Shooting, Mohamed Dassa, kwa ajili ya timu hiyo iliyopanda daraja kutoka Ligi ya Ngazi ya Wilaya na kuingia Ligi Ngazi ya Mkoa. Kombe hilo pamoja na vifaa vya michezo vimetolewa na Mbunge wa Jimbo la Korogwe Vijijini Steven Ngonyani ‘Maji Marefu
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akimkabidhivifaa vya michezo, Kiongozi wa timu ya Mombo Shooting, Mohamed Dassa, kwa ajili ya timu hiyo iliyopanda daraja kutoka Ligi ya Ngazi ya Wilaya na kuingia Ligi Ngazi ya Mkoa. Vifaa hivyo pamoja na Kombe kwa timu hiyo,  vimetolewa na Mbunge wa Jimbo la Korogwe Vijijini Steven Ngonyani ‘Maji Marefu’. 

0 maoni:

Post a Comment

WANAOTEMBELEA KWA SIKU