BINGWA wa ngumi za kulipwa anayetambuliwa na vyama vya ICB, IBF na WBC, 
Francis Cheka 'SMG' usiku wa kuamkia leo amedhihirisha kwamba hana mpinzani 
katika ngumi hizo nchini baada ya kumchapa kwa KO mpinzani wake mkubwa, Karama 
Nyilawila na kuongeza taji jingine.
Cheka alimpiga Nyilawila katika 
raundi ya sita ya pam,bano hilo lililokuwa la uzani wa Super 
BINGWA wa ngumi za kulipwa 
anayetambuliwa na vyama vya ICB, IBF na WBC, Francis Cheka 'SMG' usiku wa 
kuamkia leo amedhihirisha kwamba hana mpinzani katika ngumi hizo nchini baada ya 
kumchapa kwa KO mpinzani wake mkubwa, Karama Nyilawila na kuongeza taji 
jingine.
Cheka alimpiga Nyilawila katika 
raundi ya sita ya pam,bano hilo lililokuwa la uzani wa Super Middle la raundi 12 
lililofanyika kwenye ukumbi wa PTA, Temeke jijini Dar es Salaam na kutwaa 
ubingwa wa Mabara wa UBO uliokuwa wazi.
Pambano hilo lililohudhuriwa na 
mashabiki lukuki, lilishuhudia raundi zote tano za kwanza Nyilawila akionyesha 
kumdhibiti Cheka kwa kumchezea 'kibabe' akitumia nguvu nyingi kujihami na baadhi 
ya watu ukumbini kuamini mwisho wa tambo za Cheka zilikuwa zimewadia.
Hata hivyo raudni ya sita ilipoanza 
Cheka alionyesha amebadilika na hasa baada ya kocha wake Abdallahj Saleh 
'Komando' kupanda ulingoni na kuzungumza na bondia huyo na kumshushia kipigo 
Nyilawila, ambapo moja ya makonde matatu ya mfululizo yalimpeleka chini mpinzani 
wake.
Mwamuzi wa pambano hilo, Jerome 
Waluza alimhesabia Nyilawila ambaye alijitahidi kuinuka, lakini ghafla 
akaonyesha ishara kwamba asingeweza kuendelea na pambano hilo na ukumbi mzima 
kuripuka kwa shangwe akishangiliwa Cheka ambaye hiyo ni mara ya pili kumpiga 
Nyilawila.
Kabla ya pambano hilo lililoanza 
majira ya saa 3;40 usiku, kulikuwa na mapambano saba ya utangulizi pamoja na 
burudani ya muziki toka bendi ya Mashujaa ambao hata hivyo sio wapenzi wengi 
walioweza kuishuhudia kutokana na kuondoka ukumbini mapema.
Katika pambano la kwanza la 
utangulizi Said Mbelwa alimpiga kwa pointi Dickson Mwakipesile, Juma Kihiyo 
alipigwa kwa pointi na Ibrahim Mahokola katika pambano lililovutia kwa namna 
mabondia hao walivyoonyeshana kazi.
Pia mdogo wa Cheka, Cosmas Cheka 
alifanikiwa kuibuka na ushindi wa pointi dhidi ya Fadhil Awadh katika pamnbano 
jingine lililosisimua wengi kwa ufundi uliokuwa ukionyesha na mabondia hao, naye 
Shaaban Kilumbelumbe alimpiga kwa pointi Anthony Mathias kabla ya Safari Mbiyu 
kumpiga kwa KO ya raundi ya kwanza Khalfan Jumanne.
Michezo minginme iliwakutanisha Stan 
Kessy na Seba Temba, pambano lililoisha kwa mabondia hao kutoka sare na Hassani 
Kidebe alitolewa nishai na Deo Samwel kwa kupigwa kwa pointi.
Mgeni rasmi katika pambano hilo 
alikuwa Kamanda wa Polisi Kanda maalum ya Dar es Salaam ambaye aliutangazia umma 
kwamba kama Mlezi wa Ngumi za Kulipwa amefanikiwa kuwafuta wafadhili katika 
mchezo huo na kumtambulisha raia mmoja wa kigeni kwamba ni miongoni 
mwao.
Middle la raundi 12 lililofanyika kwenye ukumbi wa PTA, Temeke jijini 
Dar es Salaam na kutwaa ubingwa wa Mabara wa UBO uliokuwa wazi.
Pambano hilo lililohudhuriwa na 
mashabiki lukuki, lilishuhudia raundi zote tano za kwanza Nyilawila akionyesha 
kumdhibiti Cheka kwa kumchezea 'kibabe' akitumia nguvu nyingi kujihami na baadhi 
ya watu ukumbini kuamini mwisho wa tambo za Cheka zilikuwa zimewadia.
Hata hivyo raudni ya sita ilipoanza 
Cheka alionyesha amebadilika na hasa baada ya kocha wake Abdallahj Saleh 
'Komando' kupanda ulingoni na kuzungumza na bondia huyo na kumshushia kipigo 
Nyilawila, ambapo moja ya makonde matatu ya mfululizo yalimpeleka chini mpinzani 
wake.
Mwamuzi wa pambano hilo, Jerome 
Waluza alimhesabia Nyilawila ambaye alijitahidi kuinuka, lakini ghafla 
akaonyesha ishara kwamba asingeweza kuendelea na pambano hilo na ukumbi mzima 
kuripuka kwa shangwe akishangiliwa Cheka ambaye hiyo ni mara ya pili kumpiga 
Nyilawila.
Kabla ya pambano hilo lililoanza 
majira ya saa 3;40 usiku, kulikuwa na mapambano saba ya utangulizi pamoja na 
burudani ya muziki toka bendi ya Mashujaa ambao hata hivyo sio wapenzi wengi 
walioweza kuishuhudia kutokana na kuondoka ukumbini mapema.
Katika pambano la kwanza la 
utangulizi Said Mbelwa alimpiga kwa pointi Dickson Mwakipesile, Juma Kihiyo 
alipigwa kwa pointi na Ibrahim Mahokola katika pambano lililovutia kwa namna 
mabondia hao walivyoonyeshana kazi.
Pia mdogo wa Cheka, Cosmas Cheka 
alifanikiwa kuibuka na ushindi wa pointi dhidi ya Fadhil Awadh katika pamnbano 
jingine lililosisimua wengi kwa ufundi uliokuwa ukionyesha na mabondia hao, naye 
Shaaban Kilumbelumbe alimpiga kwa pointi Anthony Mathias kabla ya Safari Mbiyu 
kumpiga kwa KO ya raundi ya kwanza Khalfan Jumanne.
Michezo minginme iliwakutanisha Stan 
Kessy na Seba Temba, pambano lililoisha kwa mabondia hao kutoka sare na Hassani 
Kidebe alitolewa nishai na Deo Samwel kwa kupigwa kwa pointi.
Mgeni rasmi katika pambano hilo 
alikuwa Kamanda wa Polisi Kanda maalum ya Dar es Salaam ambaye aliutangazia umma 
kwamba kama Mlezi wa Ngumi za Kulipwa amefanikiwa kuwafuta wafadhili katika 
mchezo huo na kumtambulisha raia mmoja wa kigeni kwamba ni miongoni mwao.





0 maoni:
Post a Comment