Monday, October 8, 2012

POLISI BALAX YA JIJINI DAR ES SALAAM WAMEIBUKA MABINGWA KATIKA MASHINDANO YA TAIFA YA DARTS (TADA)

Katibu Tawala Wilaya ya Moshi Mjini , Hashimu Shimbo(kulia) akiwakabidhi Kikombe wachezaji wa klabu ya Polisi Baalax mara baada ya kuibuka mabingwa katika fainali za mashindano ya Darts Taifa(TADA) yaliyofanyika katika Hoteli ya Hugo’s Moshi Mkoani Kilimanjaro mwishoni  mwa wiki. 

POLISI Balax  ya jijini Dar es Salaam wameibuka mabingwa katika mashindano ya Taifa ya Darts (TADA) yaliyomalizika mwishoni mwa wiki Mjini Moshi, Mkoani Kilimanjaro na kujitwalia Kikombe na pesa taslimu shilingi laki tatu(300,000/=) pamoja na cheti cha ushiriki.
Polisi Balax  waliupata Ubingwa huo kwa kichapa timu ya  Friends ya jijini Daar es Saalaam 9-2 hivyo kufanikiwa kupata nafasi ya kwanza ambapo nafasi ya pili ilikamatwa na Friends ambao walizawadiwa pesa taslimu shilingi laki mbili na cheti cha ushiriki,nafasi ya tatu ilichukuliwa na VIP ya Arusha ambayo ilizawadiwa shilingi laki moja na cheti cha ushiriki.
Katika Singles(mchezaji mmoja mmoja) wanaume nafasi ya kwanza ilichukuliwa na Wambura Msira kutoka klabu ya Lugalo ya jijini Dar es Salaam ambaye alijinyakulia pesa taslimu shilingi laki mbili na cheti cha ushiriki ambapo nafasi ya pili ilichukuliwa na Syliwa Revocatus kutoka klabu ya VIP Arusha ambaye alijinyakulia pesa taslimu shilingi laki moja na nusu na cheti cha ushiriki.
Kwa upande wa Wanawake Singles mshindi wa kwanza alichukua Irene Kiluki kutoka Klabu ya  Kimanga ambaye alijinyakulia pesa taslimu shilingi laki moja na nusu pamoja na cheti cha ushiriki ambapo mshindi wa pili alichukua Vicky Mdiki kutoka Klabu ya Moshi na kujinyakulia pesa taslimu shilingi laki moja na cheti cha ushiriki
Fainali za mashindano hayo zilihudhuriwa na mgeni rasmi,Katibu Tawala Wilaya ya Moshi Mjini , Hashimu Shimbo ambaye aliwashukuru viongozi na wachezaji kwa kufanya mashindano hayo ya Kitaifa katika mji wa Moshi Mkoa wa Kilimanjaro unaonngoza kwa usafi Tanzania,pia aliipongeza Kampuni ya Bia Tanzania kwa kudhamini mchezo wa Darts na kuwaomba wasichoke kudhamini na kuendeleza mchezo huo nchini kote
Shimbo alisema Serikali iko tayari kushirikiana na wadhamini ,wadau,vilabu,Wilaya na Mikoa kurudisha mchezo wa Darts kwenye thamani yake ya zamani.

0 maoni:

Post a Comment

WANAOTEMBELEA KWA SIKU