Meneja
huduma za jamii wa Airtel Hawa Bayumi akiongea na wanafunzi wa shule ya
Buguruni Viziwi mwishoni mwa wiki hii wakati ambapo airtel walitembelea
shule ya msingi viziwi kuhamasisha upatikanaji wa vifaa vya kufundishia
pamoja na nyenzo mbalimbali kupitia mradi maalumu wa kuchangia vitabu
unaoendeshwa na Airtel kwa kushirikiana na BAMVITA, kushoto ni Mwalimu
wa shule hiyo bi Judith Kaneno akifuatiwa na Airtel Ambassador
ajulikanae kwa jina la AY( Ambwene Yessaya) kulia ni Mwalimu mkuu bi.
Winfrid Jeromia.
Mwalimu wa shule ya msingi Buguruni
Viziwi akiwapa ujumbe wanafunzi wa shule hiyo baada ya kutembelewa na
wafanyakazi wa Airtel, kutoka kushoto ni mwamlimu mkuu wa shule hiyo bi
Winfrid Jeromia, akifuatiwa na Meneja huduma za jamii wa Airtel Hawa
Bayumi na Airtel Ambassador Ambwene Yessaya (AY). Airtel kwa
kushirikiana na BAMVITA wanaendesha mradi maalum utakaowezesha wanafunzi
hao wenye uhitaji maalum kupata vifaa vya kujifunzia
Meneja
huduma za jamii wa Airtel Hawa Bayumi akiangalia ujuzi wa wanafunzi wa
shule ya Buguruni viziwa alipotembelea shule hiyo mwishoni mwa wiki hii.
wakati AIRTEL na Balozi wao msanii AY walipofanya ziara maalum ya
kuhamasisha jamii kuchangia wanafunzi hao wa shule ya msingi Buguruni
viziwi kupata vifaa vya kujifunzia kwa kushirikiana na BAMVITA
Balozi wa Airtel nchini Ambwene
Yessaya (AY) (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na wanafunzi wa
chekechea ya shule ya msingi Buguruni Viziwi walipotembelea shule hiyo
mwishoni mwa wiki hii.Airtel kwa kushirikiana na BAMVITA wanaendesha
mradi maalum utakaowezesha wanafunzi hao wenye uhitaji maalum kupata
vifaa vya kujifunzia
0 maoni:
Post a Comment