Mchezo
wa Ligi Kuu ya Vodacom kuwania ubingwa wa Tanzania Bara kati ya Yanga
na Ruvu Shooting uliopangwa kuchezwa kesho (Oktoba 20 mwaka huu) Uwanja
wa Chamazi sasa umehamishiwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kuanzia saa
10.15 jioni.
Mabadiliko
hayo yamefanyika kutokana na maombi ya timu hizo mbili kutaka mechi
ichezwe Uwanja wa Taifa kutokana na sababu mbalimbali ambazo zimeridhiwa
na Kamati ya Ligi ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)
ikiwemo siku hiyo uwanja huo kutokuwa na mechi.
Viingilio
katika mechi hiyo itakayokuwa chini ya mwamuzi Amon Paul kutoka Mara ni
sh. 5,000 viti vya kijani na bluu, sh. 8,000 viti vya rangi ya chungwa,
sh. 15,000 VIP B na C na sh. 20,000 kwa VIP A.






0 maoni:
Post a Comment