Mechi
ya mchujo ya Kombe la Afrika kwa vijana wenye umri chini ya miaka 17
kati ya Tanzania (Serengeti Boys) na Congo Brazzaville iliyochezwa juzi
(Novemba 18 mwaka huu) Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam imeingiza sh.
23,021,000.
Mapato
hayo yametokana na washabiki 18,022 waliokata tiketi kushuhudia pambano
hilo kwa viingilio vya sh. 10,000, sh. 5,000, sh. 2,000 na sh. 1,000.
Washabiki 15,850 walikata tiketi za sh. 1,000.
Asilimia
18 ya mapato hayo ambayo ni sh. 3,511,677.97 ilikwenda kwenye Kodi ya
Ongezeko la Thamani (VAT) wakati gharama kabla ya mgawo zilikuwa tiketi
(sh. 5,956,635), usafi na ulinzi (sh. 2,350,000), maandalizi ya uwanja-
pitch preparation (sh. 400,000), Wachina- Beijing Construction (sh.
2,000,000), umeme (sh. 300,000) na ulinzi wa mechi (sh. 3,500,000).
Kwa
upande wa mgawo asilimia 20 ya gharama za mechi ni sh. 1,000,537,
asilimia 10 ya uwanja sh. 500,269, asilimia 5 ya Shirikisho la Mpira wa
Miguu Afrika (CAF) sh. 250,134, asilimia 45 ya Mfuko wa Maendeleo ya
Mpira wa Miguu (FDF) sh. 2,251,209, asilimia 20 ya TFF (sh. 1,000,537)
na Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) sh. 50,027.
0 maoni:
Post a Comment