Friday, December 7, 2012

TFF YASIKITISHWA NA KUONDOLEWA KWA TIMU ZA TANZANIA

 Katibu mkuu wa TFF Angetile Osiah akizungumza na waandishi wa habari
Waandishi wa habari wakiwa katika ukumbi TFF

Shirikisho La soka nchini TFF limesikitishwa  kwa timu za TAIFA ZA TANZANIA KILIMANJARO STARS na ZANZIBAR HEROUS kutolewa  katika hatua ya nusu fainali ya michuano ya TUSKER CHALLENGE CUP inayofanyika nchini UGANDA.

Katibu mkuu wa TFF ANGETILE OSIAH amesema walitengemea timu hizo zingefika fainali lakini kutoka na timu pinzani kuwa na wachezaji wenye uzoefu mkubwa timu hizo zimeshindwa kufika hatua ya fainali,lakini TFF inajipanga kuhakikisha anawalea vijana ili baadaye weweze kufanya vizuri.

Katika michuano hiyo KILIMANJARO STARS ilitolewa na UGANDA baada ya kufungwa magoli matatu kwa bila katika hatua ya nusu fainali ,sawa na ZANZIBAR HEROUS ambayo nayo ilitolewa na KENYA kwa njia ya matuta .

Mashindano hayo yanatarajia kumalizika kesho kwa ZANZIBAR na TANZANIA kucheza kutafuta mshindi wa tatu wakati fainali itakuwa kati ya KENYA na UGANDA.

0 maoni:

Post a Comment

WANAOTEMBELEA KWA SIKU