Thursday, December 6, 2012

ZANZIBAR NA TANZANIA ZATOLEWA KATIKA HATUA YA NUSU FAINALI


TIMU za TANZANIA za KILIMANJARO STARS na ZANZIBAR HEROES zimeshindwa kutinga hatua ya fainali ya mashindano ya CECAFA CHALENJI baada ya kuondoshwa katika mashindano hayo na timu za KENYA na wenyeji UGANDA.

Katika mchezo wa awali , ZANZIBAR HEROES iliweza kucheza vizuri katika mchezo wake dhidi ya HARAMBEE STARS ya KENYA na kushuhudia mchezo huo ukimalizika hadi dakika MIA na ISHIRINI zikiwa sare ya kufungana magoli MAWILI kwa MAWILI.

Mchezo huo ukaamuliwa kwaa penati ambapo HARAMBEE STARS ilipata penati NNE na ZANZIBAR ikapata  penati MBILI na hivyo kuondolewa katika mashindano haya.

Katika mchezo wa pili, Wachezaji EMMANUEL OKWI na ROBERT SSENTONGO walipeleka kilio  kwa timu ya KILIMANJARO STARS baada ya kuifungia timu yao magoli matatu kwa bila.

Kutokana na matokeo haya timu za TANZANIA za KILIMANJARO STARS na ZANZIBAR HEROES zitakutana katika mchezo wa kutafuta mshindi wa TATU  wakati UGANDA na KENYA zitakutana katika mchezo wa fainali

0 maoni:

Post a Comment

WANAOTEMBELEA KWA SIKU