Thursday, January 17, 2013

MZEE MALECELA, WAZIRI MKUU MSTAAFU SUMAYE NA JAJI MKUU MSTAAFU SAMATTA WATOA MAONI KATIBA MPYA

 Waziri Mkuu Mstaafu Mzee John Malecela akitoka nje ya ukumbi wa mikutano wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba leo (Alhamisi, Jan 17, 2013) mara baada ya kutoa maoni yake kuhusu katiba Mpya. Kushoto ni Makamu Mwenyekiti Jaji Mkuu Mstaafu Augustino Ramadhani na kulia ni Mjumbe wa Tume Waziri Mkuu Mstaafu Dkt. Salim Ahmed Salim.
 Waziri Mkuu Mstaafu Mzee John Malecela akiongea na Wajumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba aliokutana nao leo (Alhamisi, Jan 17, 2013) kutoa maoni yake kuhusu Katiba Mpya. Kulia ni Makamu Mwenyekiti Jaji Mkuu Mstaafu Augustino Ramadhani na Mjumbe wa Tume Prof. Mwesiga Baregu.
 Waziri Mkuu Mstaafu Mzee John Malecela akipata maelezo kuhusu Kitengo cha Utafiti cha Tume ya Mabadiliko ya Katiba kutoka kwa Mjumbe wa Sekretarieti ya Tume Bw. Mohammed Hamad leo (Alhamisi, Jan 17, 2013) mara baada ya kutoa maoni yake kuhusu katiba Mpya. Kushoto ni Mwenyekiti wa Tume Jaji Joseph Warioba.
 Jaji Mkuu Mstaafu Barnabas Samatta akiongea na Wajumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba aliokutana nao leo (Alhamisi, Jan 17, 2013) kutoa maoni yake kuhusu Katiba Mpya. Kulia ni Mwenyekiti wa Tume Jaji Joseph Warioba na Mjumbe wa Tume Bw. Awadh Said.
Waziri Mkuu Mstaafu Fredrick Sumaye akiongea na Wajumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba aliokutana nao leo (Alhamisi, Jan 17, 2013) kutoa maoni yake kuhusu Katiba Mpya. Kulia ni Makamu Mwenyekiti wa Tume Jaji Mkuu Mstaafu Augustino Ramadhani na Mjumbe wa Tume Waziri Mkuu Mstaafu Dkt. Salim Ahmed Salim (katikati).

0 maoni:

Post a Comment

WANAOTEMBELEA KWA SIKU