Friday, January 11, 2013

TAASISI ZA DINI ZA WASABATO, KHOJA SHIA, BARAZA LA TAASISI ZA KIISLAM WATOA MAONI KATIBA MPYA

 Wajumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Bi. Mary Kashonda na Dkt. Sengondo Mvungi wakifuatilia mkutano kati ya Tume na Jumuiya ya Kidini ya Khoja Shia Ithnaasher Jamaats uliolenga kupata maoni ya taasisi hiyo kuhusu Katiba Mpya. Mkutano huo ulifanyika katika ofisi za Tume jijini Dar es Salaam leo (Ijumaa, Jan 11, 2013).
  Mmoja wa viongozi wa Jumuiya ya Kidini ya Khoja Shia Ithnaasher Jamaats Bw. Mohamed Khalfan akitoa maoni ya Jumuiya hiyo kuhusu Katiba Mpya katika mkutano na Tume ya Mabadiliko ya Katiba uliofanyika katika ofisi za Tume jijini Dar es Salaam leo (Ijumaa Januari 11, 2013).
 Mmoja wa viongozi wa Jumuiya ya Kidini ya Khoja Shia Ithnaasher Jamaats Bw. Mohamed Dhirani akitoa maoni ya Jumuiya hiyo kuhusu Katiba Mpya katika mkutano na Tume ya Mabadiliko ya Katiba uliofanyika katika ofisi za Tume jijini Dar es Salaam leo (Ijumaa Januari 11, 2013).
   Mkuu wa Kanisa la Waadventista Wasabato (SDA), Kanda ya Mashariki Mchungaji Mark Malekana (kushoto) akitoa maoni ya kanisa lake kuhusu Katiba Mpya katika mkutano na Tume ya Mabadiliko ya Katiba uliofanyika katika Ukumbi wa Karimjee, Jijini Dar es Salaam leo (Ijumaa Januari 11, 2013).
 Kiongozi wa Kanisa la Waadventista Wasabato (SDA), Kanda ya Kusini, Dk. Joseph Bulongela akitoa akitoa maoni ya taasisi yake kuhusu kuhusu Katiba Mpya katika mkutano na Tume ya Mabadiliko ya Katiba uliofanyika katika Ukumbi wa Karimjee, Jijini Dar es Salaam leo (Ijumaa Januari 11, 2013).
 Makamu Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Mkuu Mstaafu Augustino Ramadhani akizunguma  na viongozi  Kanisa la Waadventista Wasabato (SDA) (kushoto) katika mkutano uliolenga kupata maoni ya kanisa hilo kuhusu Katiba Mpya. Mkutano huo ulifanyika katika Ukumbi wa Karimjee, Jijini Dar es Salaam leo (Ijumaa Januari 11, 2013).
Sheikh Ibrahim Ghulaam wa Baraza Kuu la Jumuiya na Taasisi za Kiislamu nchini akitoa maoni ya Baraza hilo kuhusu Katiba Mpya mbele ya Wajumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba wakati wa mkutano uliofanyika katika ukumbi wa wa Karimjee Jijini Dar es Salaam leo (Ijumaa tarehe 11, Januari, 2013).

0 maoni:

Post a Comment

WANAOTEMBELEA KWA SIKU