Yanga
iliyopiga kambi ya mazoezi kwa takribani wiki mbili mjini Antalya,
Uturuki itaanza mzunguko wa pili dhidi ya Tanzania Prisons katika mechi
itakayochezwa keshokutwa (Januari 27 mwaka huu) Uwanja wa Taifa, Dar es
Salaam.
Vinara
hao wa VPL wakiongoza kwa tofauti ya pointi tano dhidi ya Azam
wanaowafuatia wanaikabili Tanzania Prisons ambayo imetumia dirisha dogo
kuongeza wachezaji wawili akiwemo mshambuliaji mkongwe Emmanuel Gabriel.
Timu
hizo zilitoka suluhu katika mechi ya mzunguko wa kwanza iliyochezwa
Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine, jijini Mbeya. Hivyo kiu ya washabiki ni
kutaka kujua nani ataibuka mbabe kati ya timu hizo msimu huu.
Wakati
ameingiza wachezaji wawili kwenye dirisha dogo, Kocha wa Tanzania
Prisons, Jumanne Chale amempoteza David Mwantika katika dirisa hilo.
Beki huyo ametua katika timu ya Azam.





0 maoni:
Post a Comment