Thursday, May 9, 2013

DAVID MOYES AWA MRITHI WA SIR ALEX FERGUSON KWA MKATABA WA MIAKA 6

 
Bodi ya klabu ya MANCHESTER UNITED imempitisha kwa kauli moja kocha wa EVERTON DAVID MOYES kuwa kocha wa MANCHESTER UNITED kwa kuumpa mkataba wa miaka sita na ataanza kazi rasmi JULAI mosi.mwaka huu

Uteuzi huo umekuja baada ya SIR ALEX FERGUSON kutangaza kustaafu kazi ya ukocha mwishoni mwa mwezi huu .
DAVID MOYES amesema ni heshima kubwa kuteuliwa kufundisha timu  kubwa ya MANCHESTER UNITED amemshukuru FERGASON kwani yeye ndiye alipendekeza jina lake.
Kocha MOYEZII atatambulishwa rasmi katika klabu ya MANCHESTER UNITED mara baada ya kumaliza mkataba wake na EVERTON JUNE 30 mwaka  huu.

Moyez alianza kazi ya Umeneja Preston North End Januari 1998 Klabu ikiwa taabani Divisheni ya Pili na ikiwa hatarini kuporomoshwa Daraja.
Lakini Moyes, ambae alianza kuchukua Mafunzo ya Ukocha na kupata Beji zake tangu akiwa na Miaka 22 wakati akiwa Mchezaji, aliinusuru Preston kushushwa Daraja na Msimu uliofuata aliiwezeshe kutinga Mechi za Mchujo za kupandishwa Daraja lakini hawakufanikiwa.

Msimu uliofuata Moyes aliifanikisha Preston North End kutwaa Ubingwa wa Divisheni ya Pili na kupanda Daraja kuingia Divisheni ya Kwanza ambako Mwaka 2001 aliifikisha Mechi za Mchujo za kupandishwa Daraja lakini hawakufanikiwa.
Moyez alihama Preston na kwenda Everton Mwezi Machi 2002.
 

0 maoni:

Post a Comment

WANAOTEMBELEA KWA SIKU