Sunday, May 5, 2013

FAINALI YA MASHINDANO YA POOL KWA ELIMU YA VYUO VIKUU YAFANYIKA IRINGA

https://mail-attachment.googleusercontent.com/attachment/u/0/?ui=2&ik=c5efcfe0c1&view=att&th=13e749d0bf8705fa&attid=0.1&disp=inline&realattid=f_hgc6htm00&safe=1&zw&saduie=AG9B_P-2CrkZwFZoIv7yIISqZzQc&sadet=1367760533647&sads=m7XjCOfJd_hBbGVS7oT6IqW4Rts 
Diwani wa Kata ya Kitanzini Manispaa ya Iringa Mjini,Jescar Msambatavangu (wapili kushoto) akimkabidhi Kikombe nahodha wa timu ya Chuo Kikuu cha Ruaha, Said Mohamed mara baada ya kuibuka mabingwa katika fainali za mashindano ya Safari Lager Higher Learning Pool Competition 2013 yaliyomalizika mwishoni mwa wiki Mkoani Iringa.Kushoto ni Meneja wa Bia ya Safari Lager, Oscar Shelukindo na Meneja wa Kampuni ya Bia wa kanda za juu Kusini ,Raymond Degera.

CHUO kikuu cha Ruaha (Rucco), juzi kilifanikiwa kutetea ubingwa wake wa mashindano ya mchezo wa pool kwa wanafunzi wa elimu ya juu mkoani ya 'Safari Lager Higher Learning Competition 2013'  baada ya kuibuka na ushindi wa magoli 13-10 dhidi ya chuo kikuu cha Mkwawa katika mchezo wa fainali ya mashindano hayo.
Mashindano hayo yaliyoshirikisha vyuo vikuu vitatu vya mkoani hapa yanayodhaminiwa na Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) yalifanyikia kwenye ukumbi wa Twisters.
Chuo kikuu cha Ruaha kwa kutwaa ubingwa wa mkoa huo kwa wanafunzi wa elimu juu mkoani hapa mbali ya kujinyakulia fedha taslim Sh.500,000 pia kilikata tiketi ya kuuwakilisha mkoa huo katika fainali za taifa za mashindano hayo zitakazofanyika kuanzia Juni mosi mwaka huu jijini Dar es Salaam.
Nafasi ya tatu ya mashindano hayo ilichukuliwa na chuo cha Tumaini ambacho kilizawadiwa fedha taslim Sh.300,000.
Mbali ya vyuo hivyo kupata fedha hizo taslim lakini pia kila chuo kilipata mbuzi mmoja mmoja waliotolewa na diwani wa kata ya Kitanzini katika manispaa ya Iringa mjini, Jesca Msambatavangu ambaye ndiye aliyekuwa mgeni mgeni rasmi katika kilele cha mashindano hayo.
Kwa upande wa mchezaji mmoja mmoja (wanaume), Said Mohamed wa chuo cha Ruaha alifanikiwa kutetea ubingwa wake baada ya kumfunga Hamphrey  Tengie wa chuo cha Tumaini magoli 3-0.
Mohamed kwa kutwaa ubingwa huo alizawadiwa Sh.150,000 na pia kukata tiketi ya kuuwakilisha mkoa huo katika mashindano hayo ngazi ya fainali wakati, Tengie alliyeshika nafasi ya pili alizawadiwa Sh.100,000.
Na kwa upande wa mchezaji mmoja mmoja (wanawake), Hellen Kitali wa chuo cha Tumaini alitwaa ubingwa huo baada ya kumfunga Beatrice Nadafu wa chuo cha Ruaha magoli 4-3 na kujinyakulia Sh.100,000 na tiketi ya kuuwakilisha mkoa  huu katika fainali za taifa, wakati Beatrice aliyeshika nafasi ya pili aliondoka na Sh.50,000.
Zawadi zote kwa washindi zilikabidhiwa na diwani wa kata ya Kitanzini, Jesca Msambatavangu ambaye ndiye aliyekuwa mgeni rasmi.
Baada ya kukabidhi zawadi kwa washindi, diwani huyo licha ya kuwapongeza mabingwa wa mashindano hayo pia aliwataka wachezaji wa vyuo vingine ambao hawakuchukuwa ubingwa kuongeza bidii ya mazoezi ili mwakani waweze kufanya vizuri.
 

0 maoni:

Post a Comment

WANAOTEMBELEA KWA SIKU