Baada ya kutimuliwa na klabu ya QPR
kocha MARK HUGHES sasa amechakuliwa kukinoa kikosi cha STOKE CITY kwa muda wa
miezi sita.
HUGHES amechukua nafasi ya aliyekuwa
kocha wa STOKE CITY TONY PULIS, ambaye alitimuliwa
na timu hiyo wiki iliyopita baada ya kuifundisha kwa muda wa miaka saba.
MARK HUGHES, mwenye
umri wa Miaka 49 na ambae aliwahi kuzichezea Klabu za Manchester United, Barcelona
na Chelsea, alitimuliwa QPR Mwezi Novemba Mwaka jana.
Hughes alianza
kazi ya Umeneja Mwaka 1999 akiwa na Timu ya Taifa ya Wales kisha Blackburn
Rovers Mwaka 1994 na baada Miaka minne kuhamia Manchester City ambako alidumu
Miezi 18 na kubadilishwa na Roberto Mancini.
Baadae akaenda
Fulham alipokaa Msimu mmoja na kuhamia QPR Januari 2012 na kuinusuru kushushwa
Daraja lakini Msimu uliofuatia, ule wa 2012/13, Miezi mitatu tu tangu uanze,
akafukuzwa.
0 maoni:
Post a Comment