Monday, May 20, 2013

MISS TANGA KUFANYIKA JUNE 22 MWAKA HUU MKOANI TANGA



SHINDANO la mkutafuta malkia wa Mkoa wa Tanga mwaka huu "Redd's Miss Tanga 2013" litafanyika Juni 22 kwenye Uwanja wa Mkwakwani,Mkoani humo.

Akizungumza na gazeti hili jana Mkurugezi wa Kampuni ya DATK Intertaimeint, Asha Kigundula, alisema kuwa warembo tayari wameanza mazoezi yakatofanyika kwenye Ukumbi wa Lavida uliopo jijini Tanga.

Kigundula alisema shindano hilo litaanza saa 2, usiku, ikiwa ni pamoja na kuwa na burudani mbalimbali kutoka kwa moja ya bendi maarufu hapa nchini pamoja na wasanii wanaotamba katika muziki wa kizazi kipya.

Alisema maandalizi ya shindano hilo yanaendelea vizuri jumla ya warembo 14 watashindania taji hilo. Kigundula alisema kuwa mpaka juzi warembo 10 wamejitokeza na kuanza mazoezi yanayosimamiwa  Miss Tanga 2012 Teresia Kimolo na  Mwanaid Omar.

Hawa Ramadhan (18),Hazina Mbaga (19)Like Abdulraman (19), Jack Emannuel (18),Waida Mmbwambo(20), Tatu Hussein(19), Mwanahamis Mashaka(20), Neema Abdallah (18), Winfrida Gutram (21)Lulu Mbonea (19) na Aisha Rashid (21).

Redd's, Miss Tanga, imedhaminiwa na CXC Africa, Executive Solutions,Busta General Supply, Mkwabi Interprises,Lusindic Investment LTD, Lavida Pub, Jambo Leo,Staa Spoti,Five Brothers Cloud's Media Group,  pamoja na Blog Michuzi Media Group, Bongostaz.com, Saluti5,Kajuna, JaneJohn5, na Kidevu.

0 maoni:

Post a Comment

WANAOTEMBELEA KWA SIKU