Friday, May 10, 2013

WAZEE WA YANGA WAJA NA MPYA WAAHIDI USHINDI MECHI YA WATANI



Wazee wa klabu ya yanga imetoa tamko juu ya mchezo wa marudiano wa watani wa jadi ambapo wazee hao walianza kutoa pongezi kwa  Viongozi wa Klabu ya YANGA chini ya Mwenyekiti Yusuf Manji na Makamu Mwenyekiti Clement Sanga kwa kuongoza Klabu na kuweza kunyakua Ubingwa wa Ligi Kuu ya Vodacom msimu huu wa mwaka 2012/2013.

 Akizungumza kwa niamba ya wazee wenzake Ibrahim Akilimali amesema ubingwa wa yanga umetokana na Uongozi bora, uwajibikaji katika kutekeleza majukumu ya Klabu na kufikia malengo.

Mwenyekiti wetu ametujengea dhana ya kuwa na imani ndani ya Uongozi, wanachama na wachezaji wetu.Hivyo basi na sisi kama wazee wa Klabu tunayo imani na viongozi na wachezaji wetu na tunaahidi kuwa mchezo wetu wa tarehe 18 Mei 2013 kati yetu na Simba lazima tushinde ili tusherehekee Ubingwa wetu kwa furaha, shangwe na nderemo.

Sherehe haitakuwepo kama watashindwa kumfunga myama mei 18 uwanja wa taifa

“YANGA DAIMA MBELE NYUMA MWIKO”

0 maoni:

Post a Comment

WANAOTEMBELEA KWA SIKU