Tuesday, August 13, 2013

TIGO YATOA ZAWADI YA FLAT SCREEN SAMSUNG LCD KWA WATEJA WAKE WA FACEBOOK

  Mwanafunzi wa chuo cha St. Joseph, Goodluck Msongore (23) akipokea zawadi ya Samsung LCD flat screen ya inchi 40 kutoka kwa Afisa Mtandao wa Kijamii wa Tigo Bi. Samira Bamaar katika hafla fupi iliyofanyika jana. Akishuhudia ni Meneja Chapa wa Tigo Bw. William Mpinga.  Tigo imetoa flat screen hizo kama zawadi kwa washindi wa wateja wake wa Facebook waliojitokeza kushiriki mashindano ya kampuni hiyo iliyokuwa inasherekea ukarasa wake wa Facebook kufikisha zaidi ya watu 200,000 (laki 2) hivi karibuni.
  Mshindi wa pili, Steven Kisaru (22) ambaye ni mfanyakazi wa bandari Dar es Salaam akipokea kwa furaha remoti ya flat screen Samsung LCD yenye inchi 40 na thamani ya shilingi milioni 2 aliyojishindia kutoka katika ukurasa wa Facebook wa Tigo. Anayemkabidhi ni Afisa Mtandao wa Kijamii kutoka Tigo Bi. Samira Bamaar, huku Meneja Chapa wa Tigo Bw. William Mpinga akishuhudia. Katika mashindano hayo wateja wengine walijishindia simu za Samsung Galaxy S4, Ascend Y300 pamoja na modem na vocha kutoka Tigo.
 Afisa Mtandao wa Kijamii kutoka Tigo Bi. Samira Bamaar (kulia) akimkabidhi mshindi wa pili Marty Lyanga (25) flat screen aina ya Samsung LCD mpya kabisa yenye thamani ya shilingi milioni 2. Marty ni mwanafunzi wa Information Management katika chuo cha Tumaini, Dar es Salaam. Akishuhudia ni Meneja Chapa wa Tigo Bw. William Mpinga. 
Mwanafunzi wa Bandari College, Daffd Laurent (20), akionyeshea flat screen yake mpya aina ya Samsung LCD ya inchi 40 aliyejishindia katika ukurasa wa Facebook wa Tigo. Kulia ni Afisa Mtandao wa Kijamii kutoka Tigo Bi. Samira Bamaar. Tembelea ukurasa wa Tigo Facebook uweze kupata habari na kujishindia zawadi mbali mbali pitia www.facebook.com/TigoTanzania

0 maoni:

Post a Comment

WANAOTEMBELEA KWA SIKU