Monday, September 9, 2013

ISLAMIC BANKING YA NBC KUPELEKA WATEJA WAWILI NA WENZA WAO HIJJA

 Kaimu Mkuu wa Idara ya Huduma za Kibenki kwa Kufuata Kanuni za Kiislamu (Islamic Banking), wa Benki ya NBC Tanzania, Yassir Masoud (katikati) akizungumza katika droo ya awamu ya pili  kupata washindi wawili waliojishindia safari wao na wenza wao inayolipiwa kila kitu na NBC kushiriki ibada ya Hija mjini Makka nchini Saudi Arabia baadae Mwezi ujao. Hafla hiyo ilifanyika jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki. Wengine kutoka kushoto ni Meneja Masoko wa NBC, Alina Maria Kimaryo, Meneja Uhusiano wa benki hiyo, Eddie Mhina na Mkaguzi Mwandamizi wa Bodi ya Michezo ya Kubahatisha Tanzania, Humudi Abdulhussein.
 Meneja Uhusiano wa Benki ya Taifa ya Biashara (NBC), Eddie Mhina akipiga simu kwa mmoja wa washindi wa kampeni ya Islamic Banking ya benki hiyo ambayo washindi wawili na wenzao wao watalipiwa gharama zote kwenda Makka nchini Saudi Arabia kushiriki ibada ya Hijja baadae mwezi ujao. Wengine kutoka kushoto ni Meneja Masoko wa benki hiyo, Alina Maria Kimaryo, Kaimu Mkuu wa Islamic Banking ya NBC, Yassir Masoud na Mkaguzi Mwandamizi wa Bodi ya Michezo ya Kubahatisha Tanzania, Humudi Abdulhussein.
 Mkaguzi Mwandamizi wa Bodi ya Michezo ya Kubahatisha Tanzania, Humudi Abdulhussein (katikati) akihakiki majina ya washindi wa kampeni hiyo. Wengine kutoka kushoto ni Kaimu Mkuu wa Huduma za Kibenki kwa kufuata kanuni za Kiislamu wa NBC, Yassir Masoud na Meneja Uhusiano wa benki hiyo, Eddie Mhina pamoja na baadhi ya waandishi wa habari waliohudhuria hafla hiyo.
Kaimu Mkuu wa Islamic Banking ya NBC, Yassir Masoud (katikati) akifurahi pamoja na baadhi ya maofisa wa benki hiyo wakati baadhi ya washindi wakielezea furaha yao baada ya kupigiwa simu na kujulishwa kujishindia safari ya kwenda hijja itakayolipiwa kila kitu na NBC. Kutoka kushoto ni Ofisa katika Idara ya Operesheni, Edesia Kahyarara, Meneja Masoko, Alina Maria Kimaryo, Meneja Uhusiano, Eddie Mhina na  Mkaguzi Mwandamizi wa Bodi ya Michezo ya Kubahatisha Tanzania, Humudi Abdulhussein.

0 maoni:

Post a Comment

WANAOTEMBELEA KWA SIKU