Kikundi cha
Nyarusurya wakishangilia mara baada ya kuongoza wenzao na kutwaa ubingwa katika
mbio za mitumbwi zilizofanyika mwishoni mwa wiki Musoma.Picha na Mpiga Picha
Wetu.
KIKUNDI cha
Nyarusurya Group cha wapiga kasia Wanaume kutoka Musoma Mjini,kimetwaa ubingwa
wa mashindano ya mbio za Mitumbwi zinazodhaminiwa na Kampuni ya Bia nchini
kupitia Bia ya Balimi Extra Lager na hivyo kujitwalia zawadi ya fedha taslimu
Shilingi 900,000/= pamoja na tiketi ya kuwakilisha mkoa wa Mara katika
mashindano ya Kanda yanayotarajiwa kufanyika jijini Mwanza hivi karibuni.
Nafasi ya
pili ilichukuliwa na kikundi cha nahodha Bernard toka kinesi ambao walizawadiwa
fedha taslimu shilingi 700,000/= pamoja na nafasi ya kuwakilisha mkoa huo pia
katika fainali za Kanda pale jijini Mwanza ,nafasi ya tatu ilichukuliwa na
kikundi cha nahodha Benedkito Chamba kutoka Bwai ambao walizwadiwa fedha
taslimu shilingi 500,000/= , nafasi ya nne ilichukuliwa na kikundi cha Mweme
kutok a Kinesi ambao walijinyakulia zawadi ya fedha taslimu shilingi 400,000/=
na nafasi ya sita mpaka ya kumi walipewa kufuta jasho cha fedha taslimu
shilingi 250,000/= kwa kila kikundi.
Upande wa
Wanawake kikundi cha Kisorya Group kutoka Kisorya Bunda ambao walikuwa mabingwa
wa kanda mwaka jana upande wa wanawake,Kilitwaa ubingwa na hivyo kuzawadaiwa
fedha taslimu Shilingi 700,000/= pamoja na tiketi ya kuwakilisha mkoa wa
Mara,kwenye mashindano ya Kanda pale jijini Mwanza mwezi ujao.
Nafasi ya
pili upande wa wanawake ilichukuliwa na kikundi cha Nyamiti kutoka Majita ambao
walijinyakuliwa zawadi ya fedha taslimu shilingi 600,000/= pamoja na
kuwakilisha mkoa huo kwenye fainali za Kanda upande wa Wanawake pale jijini
Mwanza,nafasil ya tatu ilichukuliwa na kikundi cha Mama Lameck Kutoka Lukuba
ambao walizawadiwa fedha taslimu shilingi 400,000/=,nafasi ya nne ilichukuliwa
na kikundi chaRhob kutoka Kinesi, ambao walijinyakulia zawadi ya fedha taslimu
shilingi 300,000/= nafasi ya sita mpaka ya kumi walipewa kifuta jasho ya fedha
taslimu cha shilingi 200,000/= kila kikundi.
Akizungumza
mgeni rasmi wa mashindano hayo Ambaye ni mkuu wa upelelezi wilaya ya
Musoma,Juma Mataka wakati wa kukabidhi zawadi Mbali mbali kwa washindi wa
shindano hilo alisema kuwa Kampuni ya Bia Tanzania kwa kutambua umuhimu wa
Mashindano Hayo kupitia bia yake ya Balimi wameamua kuboresha mashindano ya
kupiga kasia ili kuwawezesha washiliki kujiingizia kipato.
Nae
Mwakilishi wa Tbl meneja mauzo wa kanda ya ziwa, Malaki Sitaki alisema
kuwa Kampuni ya Bia Tanzania imeamua kutengeza ajira kupitia mashindano
ya Kupiga kasia ili kuwawezesha wavuvi kujiingiza kipato na kuweza kuheshimika
kutokana na ajira hiyo kuwa imetupwa na watu wengi kutokana na wahusika
kuonekana katika jamii kuwa ni watu walioshindwa maisha.
Fainali za
Kanda za mashindano hayo yanatarajiwa kufanyika Decemba 7,2013, katika ufukwe
wa Mwaloni jijini Mwanza ambapo watashindana mabingwa wa Kanda nzima toka mikoa
ya Kigoma, Kagera,Ukerewe,Musoma na wenyeji Mwanza.
0 maoni:
Post a Comment