Wednesday, November 6, 2013

LOWASA ANENA

LOWASA PHOTO

WAZIRI Mkuu wa zamani, Edward Lowassa kwa mara nyingine tena ameibuka na kauli ambao alishawahi kuitoa huko nyuma ya viongozi wa Serikali ya awamu ya nne kushidwa kuchukua uamuzi mgumu kwa maslahi mapana ya taifa.

Lowassa alitoa kauli hiyo mjini Dodoma katika kikao cha bunge kinachoendelea akisema nchi inakosa viongozi jasiri wenye kusimamia utekelezaji wa mambo waliyoamua katika Nyanja mbalimbali za maendeleo.

“wananchi, wanasiasa, wabunge, viongozi wanalalamika hatuwezi kuwa na jamii ya kulalamika lazima mtu mmoja ajitokeze na kufanya maamuzi magumu lazima ajivishe joho la ujasiri ili mambo yaende,’ amesema Lowassa

Amesema nchi ina tatizo kubwa la uswahili mwingi wa kukaa na kushidwa kutekeleza mambo yaliyoamualiwa kwenye vikao kiasi cha kufanya kila mtu kulalamika kwa wakati wake

Lowassa amesema kuwa hata matokeo makubwa sasa au “Big results Now” haiwezi kutekelezwa kwa sababu ya uswahili na mazingira ya hapa Tanzania na Malaysia ni tofauti hapa ni uswahili tu ndio unaosumbua taifa letu lishindwe kusonga mbele.

“Tukishakubaliana mambo ni lazima yafanyike. Ni lazima tuondokane kuwa nchi ya kulalamika kuanzia kiongozi wa juu mpaka mwananchi,” alisisitiza

Sisi kama MOblog tunaungana na Lowassa katika kutekeleza mipango ya serikali kama ilivyopangwa bila woga wala kigugumuzi lazima viongozi wote waliopewa dhamana ya kuongoza waongoze kwa vitendo waache uswahili ili taifa liweze kusonga mbele.

<

0 maoni:

Post a Comment

WANAOTEMBELEA KWA SIKU