Friday, November 8, 2013

SAFARI LAGER YAKABIDHI TRACTOR KWA MJARIAMALI WA PROGRAM YA “SAFARI LAGER WEZESHWA”.

 Meneja wa Bia ya Safari Lager, Oscar Shelukindo akiwasha trekta wakati wa hafla fupi ya kumkabidhi mjasiliamali wa kilimo, Filemon Choroha(chini kushoto) aliyefaulu kupewa kifaa hicho katika awamu ya pili ya program ya Wezeshwa na Safari Lager.Hafla ya makabidhiano ilifanyika Dar es Salaam jana.
 Meneja wa Bia ya Safari Lager, Oscar Shelukindo(kulia) akimkabidhi mjasiliamali, Filemon Choroha kadi ya Trekta na funguo, ikiwa ni ruzuku ya program Wezeshwa na Saafari Lagar awamu ya pili ambapo mjasilamali huyo alifuzu kupewa. Hafla ya makabidhiano ilifanyika Dar es Salaam jana.
 Meneja wa Bia ya Safari Lager, Oscar Shelukindo(kulia) akimkabidhi mjasiliamali, Filemon Choroha kadi ya Trekta na funguo, ikiwa ni ruzuku ya program Wezeshwa na Saafari Lagar awamu ya pili ambapo mjasilamali huyo alifuzu kupewa. Hafla ya makabidhiano ilifanyika Dar es Salaam jana.Kushoto ni Jaji Mkuu wa Taasisi ya TABDS, Joseph Migunda, kutoka kampuni ya TABDS.
Meneja wa Bia ya Safari Lager, Oscar Shelukindo(kulia) akimkabidhi mjasiliamali, Filemon Choroha Trekta baada ya kufuzu vigezo katika awamu ya pili ya program ya Wezesha na Safari Lager. Hafla ya makabidhiano ilifanyika Dar es Salaam jana.

Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) kupitia bia yake ya Safari Lager leo imekabidhi rasmi Tractor mpya kabisa aina ya SOLANIKA DI-75 RX kwa mjasiriamali Filemoni Choroha wa mkoani Morogoro. Makabidhiano haya yamefanyika chini ya programu ya “Safari Lager Wezeshwa”.
 
Akizungumza katika hafla fupi ya kukabidhi Tractor hiyo jijini Dar Es Salaam leo Meneja wa bia ya Safari Lager Bw. Oscar Shelukindo alifafanua kwamba hii ni ruzuku ya mwisho kugaiwa kwa wajasiriamali baada ya makabidhiano mengine ya ruzuku kwa wajasiriamali yaliyofanyika katikati ya mwaka huu katika mikoa ya Arusha, Mwanza Mbeya na Dar Es Salaam.
 
Bw. Oscar alifafanua namna washindi walivyopatikana, ngazi ya kwanza ya programu hii ilihusisha wajasiriamali wadogowadogo kujaza kwa usahihi na kutuma fomu za maombi ya ruzuku. “Tunawashukuru watanzania wote kwani kulikuwa na maombi kutoka mikoa mingi sana ya Tanzania, jumla ya mikoa 23 ilishiriki zoezi hili. Hii inaonyesha wajasiriamali wa Tanzania wana muamko wa kujiendeleza na kuendeleza jamii inayowazunguka, kuwasaidia kutimiza ndoto hii ndio lengo kuu la shindano hili.”
 
Bw. Shelukindo alifafanua kwamba baada ya fomu za maombi ya ruzuku kukusanywa zilichambuliwa na majaji wenye utaalamu wa mambo ya biashara. Jumla ya fomu 11,230 zilikusanywa ambapo wajasiriamali 68 walichaguliwa. Timu ya wataalamu hawa wa biashara waliwatembelea wajasiriamali waliochaguliwa ili kuhakiki uwepo wa biashara zao na ndipo wajasiriamali 46 wakachaguliwa kupata ruzuku za mpango huu wa “Safari Lager Wezeshwa”. Ili kufikia wajasiriamali wengi kwa ukaribu zaidi, mikoa ilitengwa katika kanda nne, mafunzo na ruzuku zilikabidhiwa kwa wajasiriamali katika kanda hizi badala ya wote kukusanyika katika mkoa mmoja. Jumla ya ruzuku ya thamani ya shilingi milioni mia mbili zimegawanywa kwa wajasiriamali waliofaulu programu hii katika msimu wa pili.
 
Bwana Shelukindo aliendelea kusema, “Ili kutoa changamoto kwa wajasiriliamali hawa watumie ruzuku zao vizuri, Safari Lager tumeona tusiwatupe mara baada ya kuwapatia ruzuku. Wataalamu wamewatembelea mara kwa mara ili kuwasaidia walipokwama. Kwa mwaka huu tumetoa ruzuku nyingine zaidi kwa wajasiriamali waliofanya vizuri msimu uliopita”. Aliwataja wajasiriamali hao kwamba ni, Bibie Msumi, Benedict Matandiko, Vumilia Mtweve, Gregory Kiria, Johnson F. Mrema na Lilian Sandu Moshi.
 
Akizungumzia  ushiriki wa wajasiriamali katika zoezi hili jaji mkuu Bw. Joseph Migunda wa taasisi ya TAPBDS alisema wajasiriamali wa rika zote walijitokeza, idadi ya wanaume walioshiriki ni asilimia 62 ya washiriki wote, na wanawake ni asilimia 38. Alisema pia maombi yalitoka katika fani nyingi sana, mafundi wa aina mbalimbali kama magari, nguo na kuchonga samani za ndani, watoa huduma kama hoteli, mitandao ya mawasiliano, wazalishaji kama wa vyakula vya kusindika, kukoboa nafaka nk wote wamejitokeza kuomba kuwezeswa na Safari Lager. Alisema vigezo vilivyotumika ni mtu awe na biashara yake mwenyewe, mchapakazi na mwenye lengo la kujiendeleza na kusaidia jamii inayomzunguka. Majaji waliangalia ubunifu wa wazo la biashara, uwezo wa kujieleza na kama fomu imejazwa vizuri na ina viambatanishi vyote. Asilimia 28 ya fomu zote hazikujazwa kwa usahihi.
 
 
 
Bwana Shelukindo alimaliza kwa kuwashukuru watanzania wote kwa ushiriki huu, na aliwaomba radhi wajasiriamali ambao bado wanaendelea kutuma na ambao bado wako na fomu kwamba muda wa kurudisha umekwisha, aliwaomba watege sikio katika vyombo vya habari na watataarifiwa muda mwingine wa kutuma maombi ya Programu ya “Safari Lager Wezeshwa.”

0 maoni:

Post a Comment

WANAOTEMBELEA KWA SIKU