Mama Tunu Pinda akikaribishwa kufunga maonyesho ya wiki ya Wakinamama Wajasiriamali na Mratibu wa Kitaifa wa Programu ya kuendeleza wajasirimali wanawake Tanzania kutoka ILO, Noreen Toroka. kushoto kwa Mama Pinda ni Mwenyekiti wa MOWE, Bi Elihaika Mrema na
Mke wa Waziri Mkuu, Mama Tunu Pinda akifunga rasmi Maonyesho ya Wanawake Wajasirimali (MOWE) katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam, maonyesho hayo ya wanawake wajasiriamali yalikuwa ya wiki nzima ambapo wakinamama wanapata nafasi ya kuonyesha na kuuza bidhaa mbalimbali Usindikaji, Mvinyo, Batiki kwa wakazi wa jijini.
Mratibu wa Kitaifa wa Programu ya kuendeleza Ujasiriamali kwa wanawake Tanzania toka Shirika la Kazi Duniani (ILO) Noreen Toroka akizungumza wakati hafla ya kufunga maonyesho hayo ambapo amesema wiki nzima ilikuwa ni maonyesho wanawake toka sehemu mbalimbali nchini Bara na Visiwani wamepata wasaa wakubadilishana mawazo na mbinu za Kibiashara.
Mwenyekiti wa Kamati ya MOWE, Mama Elihaika Mrema akizungumza wakati wa kufunga maonyesho hayo ya Wajasirimali wakinamama jijini Dar es Salaam.
Mama Tunu Pinda akitembelea baadhi ya mabanda katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar.
Mama Tunu Pinda akipata maelezo kwa mmoja wa Wajasirimali Wanawake walioshiriki maonyeshio hayo.
Mgeni rasmi Mama Pinda akikabidhi vyeti kwa mmoja wa washiriki wa maonyesho (Certificate of Participation).
Mgeni rasmi Mama Pinda akiwa katika picha ya pamoja na wenyeji Wake na viongozi wa MOWE.
Mama Tunu Pinda akiserebuka na baadhi ya Wanawake Wajasiriamali wakati wa sherehe za kufunga maonyesho hayo.
.Watanzania wahimizwa kununua bidhaa zinazotengenezwa na wazawa
0 maoni:
Post a Comment