Meneja Mauzo
na Usambazaji wa TBL, Kanda ya Ziwa , Malaki Sitaki(kulia) akimkabidhi kikombe
Mwenyekiti wa Chama cha mbio za Mitumbwi Taifa, Richard Mgabo ikiwa ni zawadi
ya mshindi wa kwanza wanaume katika fainali za mashindano ya mbio za mitumbwi
yanayotarajiwa kufanyika mwishoni mwa wiki katika ufukwe wa Mwaloni jijini Mwanza kwaudhamini wa Bia ya
Balimi Extra Lager.Kushoto ni Mratibu wa Mashindano hayo, Peter Zacharia.
KAMPUNI ya
Bia Tanzania(TBL) kupitia Bia yake ya Balimi Extra Lager, leo imetangaza Zawadi
za washindi wa mashinsindano ya bio za mitumbwi zinazotarajiwa kufanyika
mwishoni mwa wiki,Desemba 7,2013, katika Ufukwe wa Mwaloni jijini Mwanza.
Akizungumza
na waandishi wa habari Meneja mauzo na usambazaji wa Kanda ya Ziwa, Malaki
Sitaki alisema bingwa wa mashindano hayo wa mwaka 2013 upande wa wanaume
ataibuka na kitita chafedha taslimu shilingi 2700,000/=, Kikombe pamoja na
medali za dhahabu.
Mshindi wa
pili atazawadiwa fedha taslimu shilingi 2300,000/=,mshindi wa
tatu,1700,000/=,mshindi wa nne 900,000/= na washindi wa 5 hadi wa kumi
watapatiwa kifuta jasho cha fedha taslimu shilingi 400,000/= kila kikundi.
Wakati
upande wa wanawake bingwa ataibuka na zawadi ya fedha taslimu shilingi
2300,000/=,Kikombe na medali za dhahabu,mshindi wa pili 1700,000/=,mshindi wa
tatu 900,000/=,mshindi wan ne 700,000/= na washindi wa 5 hadi 10 watapewa
kifuta jasho cha fedha taslimu shilingi 250,000/=
Malaki
alisema jumla ya timu 16 za wanaume na timu 11 za wanawake ziatarajia kuchuana
siku hiyo na hatimaye kuwapata mabingwa wa mwaka 2013.
Aidha Malaki
alivitaja vikundi vilivyotinga fainali upande wa wanaume kuwa ni Beach Boys
Kigongo kutoka Kigoma,Dautius Kiiza kutoka Kagera,Katonga A kutoka
Kigoma,Costantine Lusalago kutoka Mwanza,Leonard Kasunzu kutoka Mwanza,Toto
Sebastian kutoka Ukerewe,Simon Fundi kutoka Ukerewe, J.J.Buna kutoka
Mara,Makila Camp kutoka Kigoma ,Zaidock Kaiza kutoka Kagera,Daniel Mgenha
kutoka Mwanza,Totoji Mazige kutoka Mara,Benidicto Chamba kutoka ,Mara,Bernadr
Charles kutoka Mara,Emanuel Petro kutoka Kagera na mabingwa watetezi kikundi
cha Eliud Prosper kutoka Kagera
Wakati
upande wa wanawake ni kikundi cha Elizabeth Manoni kutoka Mara,Nyamiti Juma
kutoka Mara,Muhate Mwocha kutoka Ukerewe,Jenifer Elias kutoka Ukerewe,Tabu
Daudi kutoka Mwanza,Regina Kazungu kutoka Mwanza,Levina Costantine kutoka
Kagera,Salome Ernest kutoka Kagera,Mwangongo Star kutoka Kigoma,Akina Mama
Lemba kutoka Kigoma na mabingwa watetezi kikundi cha Nyamizi Deo kutoka Mara.
Mwenyekiti
wa Chama cha wakimbia mbio za mitumbwi Taifa, Richard Mgabo aliishukuru kampuni
ya Bia Tanzania kupitia Bia yake ya Balimi Extra Lager kwa kudhamini mashindano
hayo na kuwaomba waendelee kudhamini kwani hamasa yake inazidi kukua mwaka hadi
mwaka.
Aidha
Mwenyekiti alimtaja Mkuu wa Mkoa wa jiji la Mwanza, Injinia Everisto Ndikilo
ndiye anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika fainali hizo zitakazoanza kwa
maandamano na kupokelewa na Mkuu wa Mkoa huyo.
Nae mratibu
wa mashindano ya mbio za mitumbwi, Peter Zacharia aliwaomba wapenzi,mashabi hususani wakazi wa
Mwanza waje siku hiyo kushuhudia fainali hizo zitakazosindikizwa na burudani
lukuki ikiwemo Ngoma ya Bugobogobo ya Mang’ombe ga Kijiji kutoka Misungwi.
0 maoni:
Post a Comment