Thursday, January 2, 2014

MANCHESTER UNITED YAZIDI KUCHECHEMEA LIGI KUU ENGLAND



Bingwa mtetesi MANCHESTER UNITED imeendelea kusuasua baada ya kuchapwa na TOTTENHAM HOTSPUR bao mbili kwa moja katika uwanja wao wa nyumbani wa OLD TRAFFORD.

Alikuwa mchezaji Nyota wa Togo Emmanuel Adebayor alianza kuipatia timu yake bao la kuongoza dakika ya 34 ya mchezo ,wakati Manchester united wakiendelea kujiuliza mchezaji CHRISTIAN ERIKSEN aliongeza bao la pili kwa timu yao mnamo dakika ya 66 kipindi cha pili.
MANCHESTER UNITED walikuja juu dakika ya 68 mchezaji DANNY WELBECK aliifungia timu yake bao la kwanza na kuendelea kuwa na matumani ya kuweza kusawazisha.

Lakini hadi dakika tisini MANCHESTER UNITED wakalala kwa bao mbili kwa moja na kushika nafasi ya saba katika msimamo wa ligi.

Chelsea wao wameendelea kubakia nafasi ya tatu katika msimamo wa ligi baada ya kuifumua timu ya SOUTHAMPTON mabao matatu kwa bila katika mchezo uliopigwa uwanja wa ST MARYS. 
Mabao ya FERNANDO TORRES na wachezaji waliotoka benchi, WILLIAN NA OSCAR, yote katika kipindi cha pili, yalikamilisha ushindi huo wa ugenini kwa vijana wa Jose Mourinho walioendeleza matumaini yao ya kunyakua taji. 

CHELSEA walibakia nafasi ya tatu, alama moja nyuma ya MANCHESTER CITY na mbili nyuma ya viongozi ARSENAL baada ya kivumbi hicho kilichoandaliwa uwanja wa St Mary’s.

Kwa mara nyingine tena, nyota LUIS SUAREZ, alikuwa kigezo cha Liverpool pale alipowaongoza kupanda hadi nafasi nne bora za Ligi ya ENGLAND kwa kuibuka na ushindi wa mbao mawili kwa bila dhidi ya  HULL CITY.

Baada ya kupoteza mechi mbili  dhidi ya waasimu wao wa kuwania taji, MANCHESTER CITY NA CHELSEA, kikosi cha BRENDAN RODGERS kilirejelea tena utawala kupitia makali ya Suarez. 

Mlinda ngome DANIEL AGGER aliwapatia uongozi kupitia kichwa kwenye kipindi cha kwanza kabla ya Suarez kuwaduwaza mashabiki wa HULL CITY tena na mkwaju  wa adhabu katika dakika ya 50 na kutinga nyavuni.

ARSENAL walikaribisha mwaka wa 2014 na ushindi wa 2-0 dhidi ya CARDIFF CITY na kudumisha uongozi wao mwembamba kileleni mwa Ligi hiyo.

Ingawa waliweza kutamba, Arsenal walionekana kukosa ubunifu wa kupenya ngome ya  CARDIFF CITY .
ARSENAL ilianza kupata bao la kuongoza kupitia kwa mchezaji , NICHOLAS BENDTNER, aliyempumzisha, LUKAS PODOLSKI, katika kipindi cha pili.

THEO WALCOTT alihakikisha ushindani kwa kuzamisha la pili katika muda wa majeruhi huku ushindi huo ukiongezea tetesi kwamba huu huenda ukawa musimu ambao kikosi cha ARSENE WENGER, kitafanikiwa kusitisha ukame wao wa taji la ENGLAND. 

Mabao hao ya dakika za mwisho mwisho yaliwezesha Arsenal kurejea tena kileleni baada ya MANCHESTER CITY kuchukua uongozi wa muda pale walipokamilisha ushindi wa 3-2 ugenini Swansea.

FERNANDINHO aliwapatia CITY uongozi kabla ya WINFRIED BONY kusawazisha katika kipindi cha kwanza. 

YAYA TOURE NA ALEXANDER KOLAROV waliongezea wageni mabao ya pili na tatu kipindi cha lala salama kabla ya Bony kupata lake la pili dakika ya mwisho. 

Kwingineko, CRYSTAL PALACE walitoka sare ya 1-1 na NORWICH CITY nao FULHAM walijipatia matumaini ya kuepuka kushuka daraja kwa kuibuka  na ushindi wa 2-1 dhidi ya West Ham waliosalia taabani. 
STOKE CITY walilazimishwa sare ya 1-1 na wageni Everton huku akisawazisha na penalti katika muda wa ziada. 

ASTON VILLA walisherehekea ushindi nadra wa 1-0 ugenini SUNDERLAND waliobaki wakivuta mkia wa msimamo wa ligi 

Newcastle  kwa upande wao walifumuliwa bao moja kwa bila dhidi ya  wenyeji West Brom.

0 maoni:

Post a Comment

WANAOTEMBELEA KWA SIKU