Saturday, September 17, 2011

SEMINA YA COM-UNITY

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), kwa kushirikiana na Shirikisho la Mpira Duniani (FIFA) wameandaa semina ya siku tatu itakayofanyika Dar es Salaam kuanzia Oktoba 25-28, 2011 kwenye hoteli ya Peacock. 
 
Semina hiyo inalenga kuwaleta pamoja wadau wote muhimu katika maendeleo ya mpira wa miguu kwa wanawake. Wadau wakuu ni Serikali, mashirika yasiyokuwa ya kiserikali, wadhamini na wanahabari.
 
Lengo kuu ni  kutoa mwamko na kujenga uelewa zaidi wa mchango wa mpira wa miguu kwa wanawake katika jamii.
 
Pia kutambua nafasi na umuhimu wa wadau mbalimbali katika maendeleo ya mpira wa miguu kwa wanawake na pia kujadili na kubaini mipango, mikakati na michango mbalimbali inayotolewa/inayoweza kutolewa na wadau hao katika kumwendeleza mtoto wa kike na ushiriki wake katika  mpira wa miguu.
 
Semina hii inalenga kujenga stadi za mawasiliano na udhamini/masoko (marketing) ili kuliwezesha shirikisho kuzitumia na kuwavutia wadhamini na wadau wengi zaidi.
 
Semina ya Com –Unity itatoa nafasi kwa Serikali, NGOs wadhamini na wanahabari kutoa mada mbalimbali kuhusiana na michango yao na nafasi zao katika kuendeleza mpira wa miguu kwa wanawake.
 
Itahitimishwa kwa Tamasha la watoto wa kike watakaocheza katika mfumo wa wachezaji watano watano Oktoba 28 mwaka huu katika viwanja vya Karume kuanzia saa tatu asubuhi. Shule zifuatazo zitashiriki;
·        SOS
·        Ilala Boma Shule ya Msingi
·        Kurasini mahitaji maalum
·        Uhuru Mchanganyiko/Uhuru Girls
·        International School of Tanganyika
·        Almuntazir Girls Primary School
 
Mchana tunatarajia kuwa na tamasha la wazazi/akina mama kutoka timu mbalimbali zitakazoshiriki. Timu hizo zitajumuisha timu ya wanakamati wa maandalizi ya Com –Unity, viongozi wa mpira wa wanawake na wanahabari toka vyombo vyetu vya habari.
 
FIFA itagharamia wawezeshaji, wawakilishi wake, ukumbi na vifaa vitakavyotumika na maandalizi ya Tamasha. TFF itagharamia usafiri wa ndani, gharama za ushuru na kodi na gharama nyingine.
 
Kamati za Maandalizi
Kutakuwa na kamati nne za maandalizi ya Semina na Tamasha. Kamati hizo ni za uratibu wa washiriki, uandaaji na uwasilishaji wa mada, udhamini na tamasha na kamati ya habari. Wenyeviti wa kamati hizo wataunda kamati kuu.
 
Kamati ya Uratibu wa Washiriki
         Amina Karuma– Mwenyekiti
         Michael Bundala– Katibu
         Rose Kisiwa – Mjumbe
 
Kamati ya Udhamini na  Tamasha 
         Rukia Mtingwa- Mwenyekiti
         Jimmy Kabwe- Katibu
         Devota Komba-Ikandiro – Mjumbe
         Irene Mwasanga – Mjumbe
 
Kamati ya  Habari 
         Joyce Mhaville/Deo Rweyunga- Mwenyekiti
         Boniface Wambura– Katibu
         Zena Chande – Mjumbe
         Somoe Ngitu  - Mjumbe
 
Kamati ya Uratibu wa Uandaaji wa Mada 
         Sunday Kayuni- Mwenyekiti
         Juliana Yassoda- Katibu
         Devota John – Mjumbe
         Joan Minja – Mjumbe
 
Kamati Kuu
         Lina Mhando – Mwenyekiti
         Devota John Marwa – Katibu
         Amina Karuma – Mjumbe
         Rukia Mtingwa – Mjumbe
         Joyce Mhaville/Deo Rweyunga  - Mjumbe
         Sunday Kayuni – Mjumbe
 
Mshauri na Mwezeshaji wa FIFA: Henry Tandau
 
Tunaomba kutoa mwito kwa wadau wa mpira wa miguu wanawake watuunge mkono. Kamati ziko tayari kupokea ushauri, misaada ya hali na mali ili kufanikisha tamasha la watoto.
Lina Mhando
Mwenyekiti Kamati ya Semina ya Com-Unity
 

0 maoni:

Post a Comment

WANAOTEMBELEA KWA SIKU