Sunday, September 18, 2011

TWANGA KUZINDUA ALBAM YA 11 UINGEREZA

Na Andrew  Chale
BENDI ya muziki wa dansi ya Twanga Pepeta International ‘wanakisugua kisigino’ inayotamba  nchini  inatarajia kuzindua albam yake ya  11  Novemba  mwaka huu nchini Uingereza na Dar es Salaam.
Akizungumza mbele ya mashabiki wake waliofulika juzi usiku  kwenye ukumbi wa Mango Kinondoni, muimbaji, mnenguaji na kiongozi wa bendi hiyo Ruiza Mbutu alisema kua tayari maandalizi ya ablamu hiyo yameshakamilika na mpaka mwishoni mwa mwezi  ujao  itakua tayari na Novemba itazinduliwa rasmi kwa mashabiki wake nchini Uingereza  na  jijini Dar es Salaam sambamba na Tanzania nzima.
Mbutu alikua akitanga hayo huku akiwapongeza  Mkurugenzi wa bendi hiyo  Asha Baraka kwa kusherekea siku yake ya kuzaliwa sambamba na mwimbaji wa bendi hiyo  Haji Ramadhan aliyefanikiwa kuingia tano bora  kwenye shindano la kusaka vipaji vya uimbaji  Bongo star seach 2011.
“Leo ni siku ya furaha kwa wanatwanga na familia zao na furaha ya pekee ni kwa Asha Baraka amabayo leo ni siku yake ya kuzaliwa tunampongeza  pamoja na Haji Ramadhan kuingia tano bora ya BSS 2011, wadau wa Twanga kwa kuwajari na kuonyesha mapenzi yetu tunarajia kutoa albam  ya 11 itakayozinduliwa mwezi  Novemba Uingereza nah pa Dar ” alisema Mbutu.
Katika shoo hiyo Twanga waliweza kukonga nyoyo za mashabiki wake kwa kupiga vibao vinavyotamba kutoka albamu zao mbalimbali sambamba na rapa za papo kwa papo zilizokua zikiongozwa na Muimin Mwijuma.
Kwa upande wake, Asha Baraka aliwataka mashabiki kujitokeza kwa wingi kwenye bendi hiyo hasa katika vijiewe vyake  kikiwemo ukumbi maalufu wa kimataifa Club Bilicanas wanapopiga shoo  kila Jumatano sambamba na Jumamosi usiku ukumbini hapo pamoja na Jumapili mchana ndani ya viwanja vya Leaders Club.
MAPACHA WATATU KUINGIA MZIGONI RASMI.

VICHWA vipya kwenye maswala ya usanifu  ‘graphics’ na uhariri ‘editing’ kwenye  fillamu na muziki wa bongo Francis na Frank George Ntevi  ambao ni mapacha wametamba kufanya kweli kwenye anga hizo ilikuleta mabadiliko ya kweli kwenye soko la filamu na muziki wa Bongo
Wakizungu na Tanzania Daima  jana jijini Dar es Salaam, Mapacha hao walisema kua mpaka sasa wamesha  fanya kazi za kuongoza na kuihariri  filamu ya ‘The Magic Flower’ ya msanii na kiongozi wa shirikisho la wasanii  Tanzania (TAFF)Simon Mwakifamba.
“Mpaka sasa tumesha fanikiwa kuongoza filamu ya The Magic flower ni hakika itakapoingia sokoni watanzania watakubali kiwango cha filamu na utundu uliotumika kwenye filamu hiyo” walisema Mapacha hao.
Mbali na filamu hiyo pia waliweza kufanyia  graphis filamu za ‘Time after time’ iliyoigizwa na mastaa wa Bongo Izzo Bzness, Quick  Raca, Jackline  Wolper  na  filamu nyingine  ni ya  ‘My Angel’  part 1-2 ya Yusuph Mlela huku filamu zingine wanazozifanyia  graphics na editing zipo mbioni kutoka hapo baadae.
Frank na Francis ama  ‘The Squares’  wamekua wakifanya shuguli hizo za chini  ya studio ya Ntevi Pro vision ya Magomeni jijini Dar es Salaam iliyo chini ya baba yao.
Mwisho

0 maoni:

Post a Comment

WANAOTEMBELEA KWA SIKU