Tuesday, July 24, 2012

TIMU YA TAIFA YA OLIMPIKI YA TANZANIA YAWASILI KWENYE KIJIJI CHA MICHEZO HIYO, STRATFORD-LONDON

Timu ya Tanzania ya Olimpiki, imewasili kwenye kijiji cha michezo ya Olimpiki kilichopo Stratford, London, ikitokea kwenye mji wa Bradford. Timu hiyo ya Tanzania, iliweka kambi ya mazoezi katika Chuo Kikuu cha Bradford tangu walipowasili nchini Uingereza wiki mbili zilizopita, ikiwa tayari kuiwakilisha Taifa katika michezo hiyo ya Olimpiki 2012. Timu hiyo ilipokelewa na Balozi wa Tanzania, nchini Uingereza, Mheshimiwa Peter Kallaghe na maofisa wengine wa Ubalozi na kusindikizwa moja kwa moja kwenye kijiji cha michezo kilichopo Stratford, ikiwa tayari kwa maandalizi na ufunguzi rasmi wa michezo hiyo utakaofanyika siku ya Ijumaa 27/07/2012 hapa London.
Pichani, Balozi wa Tanzania, Mheshimiwa Peter Kallaghe akiwa pamoja na Wanamichezo hao watakaoiwakilisha Taifa mwaka huu katika Michezo ya Olimpiki nchini Uingereza.

0 maoni:

Post a Comment

WANAOTEMBELEA KWA SIKU