DROO ya pili ya Bahati Nasibu ya Shinda Noah inayoendeshwa na Kampuni ya Global Publishers wachapishaji wa magazeti ya Ijumaa Wikienda, Uwazi, Risasi, Amani, Ijumaa na Championi leo imewapata washindi wengine katika Viwanja vya Karume, jijini Dar.

Washindi waliopatikana katika droo hiyo na kujinyakulia zawadi tofauti ni, Rukia Vitali wa Boko, Dar (TV Flat Screen), Leah Andrew wa Mwananyamala (Simu aina ya Samsung Galaxy), Rehema Kigadye wa Tegeta (Jezi) huku wengine wakijinyakulia zawadi za papo kwa papo (kama wanavyoonekana pichani).
0 maoni:
Post a Comment