Timu za wapiga makasia za wanawake zikianza
mbio hizo za kusaka kitita cha Tsh.700,000 wakati wa mashindano ya
mitumbwi ya Balimi ngazi ya Mkoa yaliyofanyika jana Wilayani Musoma
Mkoani Mara ambapo washindi watakao wakilisha Mkoa huo ngazi ya Kanda
walipatikana.
Wasanii wa Timu ya Promosheni ya Bia ya
Balimi wakiwatumbuiza wananchi mbalimbali waliojitokeza kushuhudia
mashindano ya mitumbwi ya Balimi ngazi ya Mkoa yaliyofanyika jana
Wilayani Musoma Mkoani Mara.
Timu za wapiga Makasia kwa upande wa
wanawake Mkoani Mara zikinyoosha makasia muda mfupi kabla ya kuanza kwa
mashindano hayo yaliyofanyika jana Wialayani Musoma ambapo timu ya
Wanawake Kutoka Kisoya iliibuka washindi wakwanza na kujizolea kitita
cha Tsh.700,000.
Mabingwa wa mashindano ya Mitumbwi ya
Balimi (Balimi Boat Race) Mkoani Mara upande wa wanawake timu ya Kisorya
wakishangilia ushindi wao huo mara baada ya kuwasili ufukweni kwa
kuwaacha mbali wenzao na kuwa mabingwa wa mkoa huo na kukabidhiwa jumla
ya shilingi laki saba (700,000) kama zawadi ya ushindi wa kwanza.
Mabingwa wa mashindano ya Mitumbwi ya
Balimi (Balimi Boat Race) Mkoani Mara upande wa wanawake timu ya Kisorya
wakishangilia ushindi wao huo mara baada ya kuwasili ufukweni kwa
kuwaacha mbali wenzao na kuwa mabingwa wa mkoa huo na kukabidhiwa jumla
ya shilingi laki saba (700,000) kama zawadi ya ushindi wa kwanza.
0 maoni:
Post a Comment