SHIRIKISHO la ngumi za ridhaa nchini
limeanza matayarisho ya kuandaa mchezo wa kimataifa wa kirafiki dhidi ya ZAMBIA
utakaochezwa kesho katika ukumbi wa DDC KARIAKOO.
Katibu mkuu wa shirikisho hilo , MAKORE
MASHAGA amesema kwa mujibu wa ujumbe wa ZAMBIA , timu ya taifa ya vijana ya
nchi hiyo itawasili usiku huu na michezo kuanza kuchezwa kesho.
Mabondia wa Tanzania watakaocheza
michezo yao ya kimataifa ya kirafiki ni SAID HOFU , AMDANI ISSA , FRANK NICOLAS
, ISMAIL GALIATANO , KASSIM HUSEIN , MOHAMED CHIBUMBUI na GULUSHID RASHID.
0 maoni:
Post a Comment