KIKOSI CHA MALAWI .
SHIRIKISHO la soka kwa nchi za Afrika mashariki na
kati CECAFA , limeialika rasmi timu ya taifa ya MALAWI , kushiriki katika fainali za mashindano hayo
yaliyopangwa kufanyika nchini UGANDA kuanzia NOVEMBER 24 hadi DESEMBER 8 mwaka
huu.
CECAFA imekuwa na utaratibu wa kuzialika timu zilizo
nje ya ukanda wa Afrika mashariki na kati lengo likiwa ni kuboresha mashindano
hayo yanayofanyika kila mwaka.
Mwaliko wa nchi ya MALAWI kumethibitishwa na katibu
mkuu wa chama cha soka nchini humo, SUZGO NYIRENDA.
TANZANIA ni miongoni mwa nchi zitakazoshiriki
mashindano hayo ambapo itawakilishwa na ZANZIBAR HEROSE na KILIMANJARO STARS.
TBC itakuletea moja kwa moja mashindano haya kutoka
nchini UGANDA kuanzia tarehe November 24.
0 maoni:
Post a Comment