Meneja wa Bia ya Safari Laager, Oscar
Shelukindo(kulia) akizungumza na wakazi wa Mkoa wa Twara wakiwemo
wajasiliamali wakati wa uzinduzi wa Programu ya Safari Lager Wezeshwa
awamu ya pili katiaka viwanja vya Bima mkoani humo mwishoni mwa
wiki.Kushoto ni mmoja wa wajasilimali waliowezeshwa awamu ya kwanza,
Stumai Namanga.
KAMPUNI ya Bia Tanzania (TBL) kupitia bia yake ya Safari Lager jana ilizindua rasmi msimu wa pili wa programu ya kuwaelimisha wajasiriamali wa Mtwara juu ya “Safari Lager Wezeshwa”.
Akizungumza
na waandishi wa habari Mkoani Mwara wakati wa uzinduzi huo, Meneja wa
bia ya Safari Lager Bw. Oscar Shelukindo alisema timu ya Mabalozi 15 wa
ya kuelimija jamii imeshaanza kazi hapa Mtwara kutoa elimu kwa jamii ya
wakazi wa Mtwara hasa wafanyabiashara ndogo ndogo na wa kati juu ya
programu ya Safari Wezeshwa.
Alisema
Shelukindo, timu hiyo imetembea takribani mikoa yote ya Tanzania Bara
na sasa iko Mkoani Mtwara kwa kumalizia programu hiyo ambapo itatoa
elimu kwa wajasiliamali wa chini na wa kati juu ya Safari Lager Wezeshwa awamu ya pili.
Programu hii
ilipata mafanikio makubwa, mwaka jana iliwawezesha wajasiriamali 54
waliofaulu vizuri vigezo kwa kuwapa mafunzo ya biashara na ruzuku za
vitendea kazi mbalimbali vyenye thamani ya shilingi milioni mia mbili.
Bwana Shelukindo alisema, “Safari Lager kwa mara ya pili inawaletea wamiliki wa biashara nafasi ya kukuza biashara zao na kujiimarisha wao binafsi na jamii inayowazunguka. “Safari Lager Wezeshwa”itatoa
ruzuku nyingine ya thamani ya shilingi milioni mia mbili, hii ni katika
harakati za kukuza na kuendeleza biashara za wajasiriamali zaidi
watakaoingia na kufuzu vigezo vya program hii”. Aliendelea kusema
kwamba, nia hasa ya Safari Lager ni kuwazawadia
wajasiriamali ambao wamejitahidi zaidi na kufikia mafanikio katika kazi
wanazofanya kiasi cha kuleta manufaa kwao na kwa jamii
inayowazunguka”.Alifafanua kwamba programu hii inawalenga wajasiriamali
wadogo wadogo na sio wafanyabiashara wakubwa. Alisisitiza zaidikwamba
nia hasa ya programu hiini kutoa hamasa kwa wajasiriamali
kote
Tanzania ili wajitahidi zaidi katika shughuli wanazofanya na pia
kuwazawadia wale watakaofaulu ili waweze kufikia ndoto zao. Kama
ilivyokuwa msimu uliopita, fedha hizi hazitolewi kama fedha taslimu kwa
watakaofaulu vigezo, zinatolewa kama vitendea kazi vitakavyomsadia
mjasiriamali kulingana na kazi anayofanya.
Shelukindo alimaliza kwa kuwapa changamoto wajasiriamali kujitahidi zaidi sio tu kwa ajili ya kujishindia ruzuku za programu ya“Safari Lager Wezeshwa”
lakini kwa manufaa yao na jamii kwa ujumla. Aliwasihi wajasiriamali na
wafanyabiashara kwa ujumla kutega sikio kwa taarifa zaidi juu ya usajili
na kutembelea website ya www.wezeshwa.co.tz.
Bwana
Shelukindo alimaliza kwa kusema, “Tunatoa pongezikwa wajasiriamali kote
Tanzania, Safari Lager inatambua na kuthamini mchango wao mkubwa katika
maendeleo ya Taifa letu. Tunatoa shukrani zetu za dhati pia kwa
wanywaji wa Safari Lager, tunawaomba waendelee kuburudika na bia hii
inayoongoza Tanzania kwani ni mchango wao ndio unaofanya tunawawezesha
wajasiriamali wetu. Safari Lager ni bia kamili, inayodhihirisha mabingwa!.





0 maoni:
Post a Comment