Saturday, January 19, 2013

AZAM FC JUMAPILI HII UWANJANI DHIDI YA SOFAPAKA

Azam FC inaendelea na maandalizi ya siku saba jijini Nairobi, kesho watacheza mchezo wake wa pili dhidi ta SOFAPAKA ya Kenya kwenye Uwanja wa Nyayo.
 
Kocha mkuu wa Azam FC, Stewart Hall amesema mechi itakuwa nzuri kwake kutokana timu hizo kucheza mchezo wa aina inayofanana baada ya kuzifundisha timu hizo.
 
Stewart alisema mechi hiyo muhimu kwake itakuwa na sura tofauti kwa kukutanisha wachezaji walipata mafunzo kupitia kwake, hivyo mbinu na aina nyingine ya mchezo bado SOFAPAKA wanaitumia.
 
Naye Kocha wa SOFAPAKA David Ouma alisema kukutana na Azam FC katika mechi ya kirafiki ilikuwa moja ya mipango yao, wanatajia kucheza mchezo wa ushindani zaidi na kuwapa nafasi wachezaji wake wapya walisajiliwa hivi karibuni.
 
Timu hiyo inatarajiwa kurejea jijini Dar es Salaam siku ya Jumatano ikiwa ni siku mbili kabla ya kuanza kwa ligi kuu Tanzania mzunguko wa mwisho wa ligi utakaoanza Jan 26 mwaka huu.

0 maoni:

Post a Comment

WANAOTEMBELEA KWA SIKU