Thursday, February 7, 2013

HUYU NDIYO BONDIA MUHAMMAD ALI



Familia ya bondia Muhammad Ali imepinga vikali taarifa iliyotolewa na mdogo wake MOHAMED ALI aitwaye RAHMAN kuwa hali ya kiafya ya nguli huyo wa masumbwi ni mbaya na yuko mbioni kufariki dunia.

Rahman Ali siku ya jumapili alitoa tarifa katika mahojiano na gazeti la udaku la THE SUN kuwa kaka yake ni mgonjwa mahututi na yuko katika hali mbaya ambayo inaonesha kuwa siku zake zinahesabika na wao wamemuachia MUNGU.

Lakini hata hivyo Rahman alikiri kuwa hajamuona kaka yake tangu mwezi JULY mwaka jana kutokana na kupigwa marufuku na mke wa ALI lakini amesema amekuwa akiwasiliana na kaka yake kupitia simu ya mkononi.

Kauli ya RAHMAN imepingwa vikali na binti wa ALI, MAY ALI ambaye amesema amekuwa akiongea na baba yake mara kwa mara na siku ya jumapili mzee wake alikuwa akiangalia fainali ya Super Bowl akiwa nyumbani akivalia jezi ya timu ya Baltimore Ravens.

MOHAMMED ALI mwenye umri wa miaka 71 anasumbuliwa na ugonjwa wa kiharusi

0 maoni:

Post a Comment

WANAOTEMBELEA KWA SIKU