Thursday, February 7, 2013

NIGERIA NA BURKINAFASO KUKUTANA FAINALI

Timu ya NIGERIA imetinga fainali ya michuano ya AFCON baada ya kuifunga timu ya MALI bao mnne kwa moja na timu ya BURKINAFASO nayo imetinga fainali baada ya kuifunga GHANA kwa mikwaju ya penati.



Nusu  fainali ya  kwanza ilizikutanisha timu za NIGERIA na MALI ambapo katika mchezo huo timu ya NIGERIA  imefanikiwa kufika fainali ya kombe la AFRIKA kwa mara ya kwanza tangu mwaka 2000 baada ya kuifunga MALI bao 4 kwa 1 katika mchezo wa nusu fainali ya kombe hilo kwenye uwanja wa MOSES MABHIDA.

Kipindi cha kwanza ndicho kilichoihakikishia NIGERIA nafasi katika fainali ya kombe hilo kwa mwaka huu baada ya kwenda mapumziko ikiwa na faida ya bao 3 bila majibu mabao yakifungwa na ELDERSON ECHIEJILE, BROWN IDEYE na EMMANUEL EMENIKE.

Kwenye kipindi cha pili AHMED MUSA alihitimisha karamu ya magoli kwa kufunga bao la 4 kwenye dakika ya 60 na hivyo kuipatia NIGERIA ushindi huo mnono wa bao 4 kwa 1 ambapo bao la kufutia machozi la MALI limefungwa na CHEICK FANTAMADY kwenye dakika ya 75.

NIGERIA sasa itakumbana na BURKINAFASO ambayo kwa mara ya kwanza imeingia katika fainali baada ya kuifunga GHANA kwa changamoto ya mikwaju ya penati kufuatia timu hizo kutoka sare ya kufungana bao moja kwa moja katika dakika 120.

GHANA ndiyo walioanza kupata bao la kuongoza kwa mkwaju wa penati kwenye dakika za mwanzo kupitia kwa MUBARAKA WAKASO lakini BURKINABE waliokua wakionesha nia ya kutaka kufika katika fainali hiyo walifanikiwa kusawazisha kwenye dakika ya 60 kupitia kwac ARISTIDE BANCE ambaye alikosa nafasi nyingi za kufunga.

Timu hizo hazikufungana kwenye dakika 30 za nyongeza lakini mchezaji muhimu wa BURKINAFASO JONATHAN PITROIPA alipewa kadi ya pili ya njano kwa kosa la kumdanganya mwamuzi na hivyo kutoka nje ambapo ataikosa mchezo wa fainali.

0 maoni:

Post a Comment

WANAOTEMBELEA KWA SIKU