Shirikisho
la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) linawaka washabiki wa mpira wa miguu
kujitokeza kwa wingi wikiendi hii kuzishangilia timu za Azam na Simba
zitakazocheza mechi za mashindano ya Afrika jijini Dar es Salaam.
Nguvu
ya washabiki ni muhimu katika kuziweza timu hizo kufanya vizuri katika
mechi hizo za nyumbani dhidi ya Al Nasir Juba ya Sudan Kusini na Club
Libolo ya Angola.
Azam
itacheza Jumamosi (Februari 16 mwaka huu) dhidi ya Al Nasir katika
mechi ya Kombe la Shirikisho wakati Simba itaikabili Club Libolo kwenye
mechi ya Ligi ya Mabingwa Afrika itakayofanyika Jumapili. Mechi zote
zitachezwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
0 maoni:
Post a Comment