Friday, May 24, 2013

MBIO ZA HISANI ZA MBUZI 2013 ZAKARIBIA

https://mail-attachment.googleusercontent.com/attachment/u/0/?ui=2&ik=c5efcfe0c1&view=att&th=13ed6b87b3cc46ed&attid=0.1&disp=inline&realattid=f_hh3ee4d40&safe=1&zw&saduie=AG9B_P-2CrkZwFZoIv7yIISqZzQc&sadet=1369422417198&sads=XBrvJzRMZiKfAcoQNCd8EQ0lPAY 
Mwenyekiti wa Mbio za Mbuzi za Hisani Dar es Salaam, Karen Stanley (katikati) akizungumza jijini Dar es Salaam kuhusu maandalizi yam bio hizo zinazotarajiwa kutimua mbuzi jijini humo Juni 1 mwaka huu katika Viwanja vya The Green, Barabara ya Kenyatta jijini humo. Wengine ni wawakilishi wa baadhi ya wadhamini wa mbio hizo. 

WAANDAAJI  wa Mbio za Hisani za Mbuzi Dar wanatoa wito kwa umma kuyaunga mkono mashirika waliyoyachagua kwa mwaka huu.

Hadi sasa ni mashirika ya hisani tisa yameshachaguliwa ili yanufaike kutokana na fedha zitakuzopatikana katika mbio hizo mwaka huu zitakazo saidia kliniki inayowafuata wahitaji waliko (mobile health clinic), basi kwa watoto wenye ulemavu, kompyuta kwa yatima na mafunzo kwa wanawake walemavu ya kutengeneza urembo.

Waandaaji wanatumaini kusaidia vituo na mashirika zaidi ya hisani, lakini hilo litawezekana kutokana tu na idadi ya watu watakaohudhuria tukio hilo la Juni Mosi mwaka huu, na kiwango cha fedha kitakachokusanywa siku hiyo.

Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi, Karen Stanley alisema: “Fedha zitakazopatikana ni za muhimu sana katika kudumu kwa mashirika madogo madogo ya hisani yanayohangaika kutafuta fedha za kutosha kwa ajili ya miradi muhimu.

“Mwaka jana tuliweka rekodi kwa  kukusanya Shilingi 115 milioni, shukrani kwa wahudhuriaji 4,200 waliolipia getini. Kiasi hiki kilitosha kuongeza idadi ya wanufaika kufikia mashirika ya hisani 15.

“Mwaka huu tunatumaini kufanya vyema zaidi na kuwasaidia wengi wenye mahitaji, lakini inategemea na idadi ya watakaojitokeza siku hiyo.”

Tangu kuanzishwa kwake mwaka 2001, mbio hizi za hisani za kila mwaka zimekwisha kusanya zaidi ya Shilingi 660 milioni kwa ajili ya mashirika 60 ya hisani madogo madogo. 

Mbio za mwaka huu pia zitatoa vifaa vya kitaalamu kwa ajili ya watoto waliozaliwa na mtindio wa ubongo, pampu za maji na matenki kwa yatima na wanawake masikini na pia kwa mradi wa vijana wa Ukimwi. (tazama orodha ya mashirika hayo chini.)

Mama Stanley alisema: “Kila mwaka tunajaribu kadri tuwezavyo kuhakikisha kuwa fedha tunazozikusanya kupitia mbio hizi zinagawanywa kwa vikundi vinavyostahili.

“Huku uhisani likiwa ndio lengo letu kuu, tusingefanikiwa bila kuungwa mkono na wadhamini wa mbio hizi Southern Sun, Coca-Cola, Tanzanian Breweries Limited, Mantra Tanzania, Erolink, FNB na Symbion. Ni lazima pia tuzipeleke shukrani zetu kwa kampuni ya ndege ya SWISS kwa kutoa tiketi mbili za ndege kwa ajili ya bahati nasibu.

“Mwaka huu tuna zaidi ya wadhamini 50 waliotoa huduma yenye thamani na ya kifedha pia. Ni uungaji mkono wao uliotuwezesha kuiandaa siku hii ya kuvutia, lakini kila anayedhani kuwa atakuja siku hiyo anapaswa kujua kwamba tendo lake lolote hata la kununua tiketi tu litawasaidia watu wa Tanzania wenye mahitaji.”

Mbio za Hisani za Mbuzi zitafanyika Juni 1 eneo la The Green Mtaa wa Kenyatta, kuanzia saa sita mchana hadi saa 11.30 jioni. Gharama ya tiketi ni Shilingi 5,000 kwa kila mtu wa umri wowote na zitauzwa getini. Kwa maelezo zaidi tembelea tovuti yetu; www.goatraces.com

0 maoni:

Post a Comment

WANAOTEMBELEA KWA SIKU