Friday, June 28, 2013

KITAYOSCEN YATINGA NUSU FAINALI

Klabu ya KITAYOSCE FC imekuwa ya kwanza kutinga katika hatua ya Nusu Fainali ya Michuano ya Mkombozi Cup 2013 baada ya kuinyuka Nazareth ya Majengo Mjini Moshi mkoani Kilimanjaro kwa mabao 3-0.

Bao la mapema kabisa la KITAYOSCE FC lilifungwa katika dakika ya 4 ya mchezo baada ya piga nikupige langoni mwa Nazareth na kumpa mwanya Festo Antony Kiwale kutupia.
Kipindi cha kwanza kilimalizika kwa KITAYOSCE FC wakiwa mbele kwa bao 1 kwa bila huku Nazareth wakijutia nafasi walizozipata na kushindwa kuzitumia.

Katika dakika ya 17 mlinzi wa kushoto wa Timu ya KITAYOSCE FC  Annuary Mkondo alionekana kutaka kutokana na matatizo ya kifua, ndipo akaingizwa kiungo Awadhi Gumbo ambaye alienda kubadili nafasi ya Kuingo mkabaji MeshaCollins alieenda safu ya kulia ya Ulinzi na Petro Mwaipopo akienda kushoto.

Dakika ya 31 ya mchezo wa leo uliochezwa katika uwanja wa Mandela katika kata ya Pasua, mjini Moshi Kiungo wa KITAYOSCE FC Florence Florence alivalia jezi namba 10 ambaye pia ni nahodha wa klabu hiyo yenye maskani yake katika kata ya Soweto alionyeshwa kadi ya njano baada ya kumtendea vibaya mchezaji wa Nazareth wakati wakikabana.

Pia katika dakika ya 39 Nazareth walifanya mabadiliko wakimtoa  Mlinzi wa Kati John Mariki aliyeonekana kuchoka na kuingizwa Deo Lyimo ili kuongeza nguvu.

Hadi dakika 45 za kipindi cha kwanza zinamalizika KITAYOSCE FC ilikuwa mbele kwa bao moja huku wakionekana kuchez achini ya kiwango katika kipindi hicho.

Kipindi cha Pili kilianza kwa mashambulizi makali kwenye lango la Nazareth ambapo Kocha Hamad Haule wa KITAYOSCE FC alibadilisha mbinu ya kucheza kwa timu yake ambapo ilionekana kuelewana zaidi.

Mashambulizi hayo yalizaa matunda kunako dakika ya 58 ambapo Kiungo Florence Florence alipiga shuti la mbali liliomzidi mlinda mlango wa Nazareth FC Hamidu Khalifa.

Hata hivyo Nazareth walijitahidi kuweza kuzima wakati mwingine wakijaribu kutoka mbali lakini walijikuta wakizidiwa na kuishiwa nguvu kabisa kunako dakika ya 72 pale David Maganga alipofanya kazi ya ziada kwa kuwakimbiza walinzi wa Nazareth na kumtungua mlinda mlango na kufanya KITAYOSCE FC kuongoza kwa mabao 3-0.

KITAYOSCE FC ilifanya mabadiliko katika dakika za 79 na 85 kwa kuwatoa viungo Victor Nduzero na Juma Salehe na kuwaingiza David Brand na Fredrick Temba ambapo mabadiliko hayo yaliweza kuongeza ladha ya mchezo, uwanjani hapo.

Leo katika Robo Fainali ya Pili ni Mshindi wa Kundi B ambaye ni Soweto FC atachuana vikali na Golani FC mechi itakayochezwa katika Uwanja wa King George Memorial.

0 maoni:

Post a Comment

WANAOTEMBELEA KWA SIKU