Tuesday, September 10, 2013

IRINGA ,MBEYA NA DODOMA WAPATA MABINGWA WA SAFARI POOL NGAZI YA MIKOA.

 Afisa ushirika wa mkoa wa Iringa, John Kiteve wa (wa pili kulia) akimkabidhi kikombe nahodha wa klabu ya Garden, Said amaohamed, mara baada ya kuibuka mabingwa katika fainali za mashingano ya Safari Pool Taifa ngazi ya mkoa yaliyomalizika mwishoni mwa wiki mkoani humo.Kulia ni Meneja mauzo wa Mkoa wa Iringa, Philipo Kabecha na Meneja wa Bia ya Safari Lager, Oscar Shelukindo.
 Afisa ushirika wa mkoa wa Iringa, John Kiteve(kulia) akimkabidhi kitita cha fedha taslimu shilingi 700,000/= nahodha wa klabu ya Garden , Said Mohamed mara   baada ya kuibuka mabingwa katika fainali za mashingano ya Safari Pool Taifa ngazi ya mkoa yaliyomalizika mwishoni mwa wiki mkoani humo.Kulia ni Meneja wa Bia ya Safari Lager, Oscar Shelukindo.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mbeya, Diwani Athumani(wa pili kushoto) akimkabidhi nahodha wa timu ya Royal Zambezi, Emmanuel Joram, kitita cha fedha taslimu shilingi 700,000/= mara baada ya kuibuka mabingwa katika fainali za mashindano ya Safari Pool Taifa ngazi ya mkoa yaliyomalizika mwishoni mwa wiki mkoani humo.

MIKOA ya Iringa, Mbeya na Dodoma  hatimaye imehitimisha fainali za mashindano ya Safari Pool Taifa ngazi ya mikoa na kupata mabingwa wataowakilisha mikoa hiyo kwenye fainali za kitaifa zinazotarajiwa kufanyika mkoani Morogoro.
Mkoa wa Iringa upande wa timu,klabu ya  Garden ilifanikiwa kutwaa ubingwa kwa kuifunga klabu ya Ngija Masters 13-9 hivyo kuzawadiwa kitita cha fedha taslimu shilingi 700,000/= pamoja na tiketi ya kuwakilisha mkoa wa Iringa kwenye fainali za kitaifa mkoani Morogoro

Upande wa mchezaji mmoja mmoja wanaume(Singles), Goodlover Ntalande kutoka klabu ya Garden alifanikiwa kutwaa ubingwa wa mkoa kwa kumfunga Emmanuel Joseph 5-2,na hivyo kujinyakulia zawadi ya fedha taslimu shilingi 350,000/= pamoja na kuwakilisha mkoa katika fainali za kitaifa mkoani Morogoro.

Upande wa mchezaji mmoja mmoja wanawake, Naomi Ngede kutoka klabu ya Garden alitwaa ubingwa kwa kumfunga Anna Elly 3-1, na kuzawadiwa fedha taslimu shilingi 250,000/= pamoja na tiketi ya kuwakilisha mkoa wa Iringa kwenye fainali za kitaifa mkoani Morogoro.

Mkoa wa Dodoma,klabu ya  Atlantic ilifanikiwa kutwaa ubingwa  hivyo kwa kuifunga klabu ya Frolida na hivyo kuzawadiwa kitita cha fedha taslimu shilingi 700,000/= pamoja na tiketi ya kuwakilisha mkoa wa Dodoma  kwenye fainali za kitaifa mkoani Morogoro.
Upande wa mchezaji mmoja mmoja wanaume(Singles), Mohamed Idd alifanikiwa kutwaa ubingwa wa mkoa kwa kumfunga Ramadhani Issa,na hivyo kujinyakulia zawadi ya fedha taslimu shilingi 350,000/= pamoja na kuwakilisha mkoa katika fainali za kitaifa mkoani Morogoro.

Upande wa mchezaji mmoja mmoja wanawake, Zainabu Salum alitwaa ubingwa kwa kumfunga Monica Siimule, na kuzawadiwa fedha taslimu shilingi 250,000/= pamoja na tiketi ya kuwakilisha mkoa kwenye fainali za kitaifa mkoani Morogoro.

Mkoa wa Mbeya,klabu ya  Royal Zambezi ilifanikiwa kutwaa ubingwa kwa kuifunga klabu ya Shooters 13-2,na  hivyo kuzwadiwa kitita cha fedha taslimu shilingi 700,000/= pamoja na tiketi ya kuwakilisha mkoa wa Mbeya kwenye fainali za kitaifa mkoani Morogoro
Upande wa mchezaji mmoja mmoja wanaume(Singles), Daniel Mbaga kutoka klabu ya Royal class alifanikiwa kutwaa ubingwa wa mkoa kwa kumfunga Gibson Godwin 4-2,na hivyo kujinyakulia zawadi ya fedha taslimu shilingi 350,000/= pamoja na kuwakilisha mkoa wa Mbeya katika fainali za kitaifa mkoani Morogoro.

Upande wa mchezaji mmoja mmoja wanawake, Rachel Richard kutoka klabu ya Kontena Tunduma alitwaa ubingwa kwa kumfunga bingwa wa mwaka jana, Betty Sanga 3-2, na kuzawadiwa fedha taslimu shilingi 250,000/= pamoja na tiketi ya kuwakilisha mkoa  kwenye fainali za kitaifa mkoani Morogoro.

Akizungumza na wachezaji pamoja na wakazi wa Mbeya,Meneja wa Bia ya Safari Lager,Oscar Shelukindo aliipongeza mikoa yote 17, kwa kumaliza vyema fainali za mashindano hayo ngazi ya mikoa na hivyo kuviomba vilabu kujiaandaa kwa kwa muda uliobaki kwa fainali ya kitaifa.

Shelukindo aliisisitiza nidhamu katika mchezo ndio siri ya kila kitu katika mafanikio mbele ya safari huko wanakoelekea kwenye fainali za kitaifa.Vilabu 17 kutoka mikoa 17 vinatarajia kuchuana mkoani Morogoro na mwisho tutapata bingwa wa Safari National Pool Championship 2013. 

Fainali za kitaifa zinatarajiwa kufanyika katika Mkoa wa Morogoro kuanzia Septemba 19 hadi 23,mwaka huu.

0 maoni:

Post a Comment

WANAOTEMBELEA KWA SIKU