Friday, September 6, 2013

MBEYA WAANZA RASMI FAINALI ZA SAFARI POOL TAIFA

 Baadhi ya wachezaji wanaoshiriki  fainali za mashndano ya Safari Pool Taifa ngazi ya mkoa, Mkoa wa Mbeya wakiwa kwenye maandamabo kuingia ukumbini  wakati wa ufunguzi wa fainali hizo zinazofanyika Airport Pub mkoani humo. 
 Meneja matukio wa TBL tawi la Mbeya, Godfrey Mwangugulu(kushoto) akizungumza na wachezaji  wa Pool (hawapo pichani) wakati wa ufunguzi wa fainali za mashindano ya Safari Pool Taifa ngazi ya mkoa yanayofanyika Airport Pub mkoani humo.Wengine kushoto kwake ni mratibu wa mashindano hayo, Peter Zacharia,Afisa michezo wa Mkoa wa Mbeya, George Mbijima na Mwenyekiti wa chama cha Pool Mkoa wa Mbeya, Samweli Aron.
 Afisa michezo wa Mkoa wa Mbeya, George Mbijima akizungumza na wachezaji wa Pool(hawapo pichani) wakati wa ufunguzi wa fainali za mashindano ya Safari Pool Taifa ngazi ya mkoa yanayofanyika Airport Pub mkoani humo.Kulia ni Meneja  matukio wa TBL tawi la Mbeya, Godfrey Mwangugulu,mratibu wa mashindano Peter Zacharia na Mwenyekiti wa chama cha Pool Mkoa wa Mbeya, Samweli Aron.
 Afisa michezo wa Mkoa wa Mbeya, George Mbijima akicheza  wakati wa ufunguzi wa fainali za mashindano ya Safari Pool Taifa ngazi ya mkoa yanayofanyika Airport Pub mkoani humo.Wengine wanaoshuhudia kushoto kwake ni mratibu wa mashindano , Peter Zacharia  na Meneja matukio wa TBL tawi la Mbeya, Godfrey Mwangugulu
Afisa michezo wa Mkoa wa Mbeya, George Mbijima akipigiwa makofi mara baada ya kufuangua rasmi mashindano. humo.Wengine wanaoshuhudia kushoto kwake.

FAINALI za mashindano ya mchezo wa Pool Taifa zinazodhaminiwa na Kampuni ya Bia Tanzania kupitia bia yake ya Safari Lager zimeanza rasmi jana Mkoani mbeya zikishilikisha vilabu tisa vya mkoani humo.

Akifungua fainali hizo Afisa michezo wa Mkoa wa Mbeya, George Mbijima aliwaomba wachezaji kuwa na watulivu na kuzingatia nidhamu ya mchezo ili mwisho wa fainali apatikane mshindi atakaebeba bendera ya Mkoa wa mbeya kwenye fainali za kitaifa na arudi na ushindi.

Mbijima alisema taswila ya mchezo wa Pool si nzuri sana miongoni mwa watu kwani unatazamwa kama mchezo wa wahuni na hakuna mtu mwingine wa kubalilisha zaidi ya wachezaji wenyewe,hivyo kuweni na nidhamu ili hata jamii ifike mahala itambue kumbe pool ni mchezo kama michezo mingine.

Mbijima pia aliishukuru TBL, kupitia bia ya Safari Lager kwa kuendelea kudhamini mashindano hayo kwani kwa kufanya hivyo inawafanya vijana kuepuka vitu vingi ikiwemo uhalifu,kukaa vijiweni bila kazi lakini sasa wananufaika  chochote  kutokana na zawadi wanazopata ukizingaatia michezo ni ajira,michezo burudabi na michezo ni kufahamiana.

Nae Meneja matukio wa TBL Mbeya,Godfrey Mwangugulu aliwatakia wachezaji michezo mema na yenye amani mwisho apatikane bingwa wa haki atakaye wakilisha vyema Mkoa wa Mbeya
Mwisho Mwenyekiti  alivitaja vilabu vinavyoshiriki fainali za Safari Pool Mkoa wa Mbeya kuwa ni Tunduma Kontena Klabu,Royal Zambezi Klabu,Royal Glass Klabu,Shooters klabu,Luanch time klabu,Mbeya snukers klabu,Kizota klabu,Makonde klabu na Terminal Stand klabu.

Zawadi  katika fainali hizo upande wa timu,bingwa atajnyakulia fedha taslimu shilingi 700,000/=,mshingi wa pili 350,000/=,wa tatu 200,000/= na wanne 100,000/ na timu nane zitakazoingia robo fainali zitapata kifuta jasho cha fedha taslimu shilingi 50,000/= kila moja.

Upande wa mchezaji mmoja mmoja(Singles), wanaume bingwa atapata zawadi ya fedha taslimu shilingi 350,000/=,wa pili 250,000/=,wa tatu 150,000/= na wanne 100,000/= na upande wa kinadada bingwa atajinyakulia fedha taslimu shilingi 250,000/=,wa pili 150,000/=,wa tatu 100,000/= na wanne 50,000/=.

Faainali za mashindano hayo zinatarajiwa kumailizika mwishoni mwa wiki hii ambapo mgeni rasmi atakayefunga anatarajiwa kuwa RPC wa mkoa huo. 

0 maoni:

Post a Comment

WANAOTEMBELEA KWA SIKU