Wednesday, September 4, 2013

WAZEE WA YANGA WAJA JUU KUHUSU KATIBU MPYA WASEMA HANA NAFASI YANGA



Baraza la wazee wa YANGA limesema halimtambui katibu mpya wa YANGA aliyeletwa na kumuondoa  katibu aliyekuwepo RAWLENCE MWALUSAKO kwani viongozi waliomleta wamekiuka katiba ya YANGA.

IBRAHIM AKILIMALI ambaye ni katibu wa baraza la wazee amesema wamepata taarifa za kuondolewa kwa katibu wa YANGA wa zamani RAWLENCE MWALUSAKO jambo ambalo wamepinga vikali 


Baadhi ya wazee wa YANGA wamesema walikutana na katibu mpya klabuni katika mahojiano naye akashindwa kumtaja mtu aliyemleta kufanya kazi .


Baraza la wazee YANGA limesema halikatai kuletwa viongozi wapya bali uongozi wa YANGA ufuate taaratibu za katiba ya YANGA inavyotaka ikiwemo kutoa taarifa kwa kamati mbalimbali za YANGA ili zifahamu mabadiliko katika uongozi.

Wamesema katiba ya YANGA inataka kiongozi yoyote awe ni mwanachama halali wa YANGA na anafahamu taratibu za YANGA ndipo atafanya kazi

0 maoni:

Post a Comment

WANAOTEMBELEA KWA SIKU