Hamad
Yahya Juma wa Mtibwa Sugar ndiye Mwenyekiti wa kwanza wa Bodi ya Ligi
Tanzania (Tanzania Professional League- TPL Board) baada ya kushinda
katika uchaguzi uliofanyika leo mchana (Oktoba 25 mwaka huu) kwenye
ukumbi wa mikutano uliopo Golden Jubilee Tower, Dar es Salaam.
Juma
ambaye hakuwa na mpinzani alipata kura zote kumi za ndiyo zilizopigwa
na klabu za Ligi Kuu zilizohudhuria mkutano huo. Klabu ambazo
hazikuhudhuria uchaguzi huo ni JKT Ruvu, Mgambo Shooting, Coastal Union
na Rhino Rangers.
Naye Said Muhammad Said Abeid ambaye pia hakuwa na mpinzani amechaguliwa kuwa Makamu Mwenyekiti kwa kupata kura zote za ndiyo.
Kwa
upande wa wajumbe wawili wa Kamati ya Uendeshaji, wote Kazimoto Miraji
Muzo wa Pamba na Khatib Omari Mwindadi wa Mwadui wameshinda kwa kura
zilizopigwa na klabu za Ligi Daraja la Kwanza (FDL).
Muzo
alipata kura 15 za ndiyo wakati mbili zikimkataa, huku Mwindadi akipata
kura 16 na moja ilimkataa. Klabu za FDL ambazo hazikuhudhuria uchaguzi
huo ni Transit Camp, Burkina Faso, Polisi Mara, Stand United, Toto
Africans, Polisi Tabora na Kanembwa JKT.
MSUMBIJI U 20 WATUA KUIKABILI THE TANZANITE.
Timu
ya Taifa ya wanawake kwa vijana wenye umri chini ya miaka 20 imewasili
nchini leo (Ijumaa, Oktoba 25 mwaka huu) saa 8.45 mchana tayari kwa
mechi ya kwanza ya raundi ya kwanza ya Kombe la Dunia dhidi ya Tanzania
itakayofanyika kesho (Jumamosi).
Msumbiji
imetua Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) kwa ndege
ya LAM ikiwa na msafara wa watu 25 unaohusisha wachezaji, benchi la
ufundi na viongozi, na kwenda moja kwa moja kwenye hoteli ya Sapphire.
Msumbiji
ilitarajia jioni hii (saa 11) kufanya mazoezi yake ya kwanza na ya
mwisho ikiwa nchini kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Kwa
upande wa The Tanzanite, Kocha Rogasian Kaijage amesema wamejiandaa
vizuri na wako tayari kwa ajili ya mechi hiyo ambayo matokeo yake ndiyo
yatakayoamua mikakati yake kwa ajili ya mechi ya marudiano itakuwaje.
Viingilio
kwa mechi hiyo ni sh. 1,000 kwa viti vya rangi ya kijani, bluu na rangi
ya chungwa. Viingilio vingine ni sh. 2,000 kwa VIP C, sh. 5,000 kwa VIP
B wakati VIP A itakuwa sh. 10,000. Tiketi zitauzwa katika magari
maalumu uwanjani.
Naye
Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Leodegar Tenga
amewataka Watanzania kujitokeza kwa wingi uwanjani ili kuiunga mkono The
Tanzanite ili iweze kufanya vizuri kwenye mechi hiyo.
TUNAFURAHI KUSIKIA AJENDA- TENGA.
Rais
wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) anayemaliza muda wake,
Leodegar Tenga amesema amefurahishwa na jinsi kampeni za uchaguzi
zinazokwenda kutoka na ukweli kuwa wagombea wamekuwa wakielezea kile
wanachotaka kuufanyia mpira wa miguu.
Akizungumza
na waandishi wa habari kwenye ofisi za TFF leo mchana, Rais Tenga
ambaye pia ni mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la Mpira wa
Miguu Afrika (CAF) amesema Watanzania wanataka kusikia ajenda za
wagombea.
“Ombi
langu ni kwamba kampeni zimeanza vizuri, watu wanazungumza hoja zaidi.
Ni jukumu la wajumbe kupima na kufanya uamuzi. Kwangu mimi
nimejitayarisha kumkabidhi Katiba, Rais mpya wa TFF,” amesema.
Tenga
ambaye pia ni Mwenyekiti wa Baraza la Vyama vya Mpira wa Miguu Afrika
Mashariki na Kati (CECAFA) amesema kazi kubwa iliyofanywa na uongozi
wake ni kujenga taasisi (TFF) pamoja na kuweka mifumo (structure)
inayoainisha majukumu ya kila mmoja.
“Ajenda
yetu wakati tunaingia madarakani mwaka 2005 ilikuwa ni kujenga taasisi.
Tayari taasisi ipo, sasa mtazamo uwe kuushughulia mpira wa miguu
wenyewe,” amesema.
Mkutano
Mkuu wa TFF unafanyika kesho kwenye ukumbi wa mikutano wa NSSF
Waterfront, na tayari wajumbe wa mkutano huo ambao pia utakuwa na ajenda
ya uchaguzi siku inayofuata wameshawasili jijini Dar es Salaam.
Wawakilishi
kutoka Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA), Ashford
Mamelodi ambaye ni Ofisa Maendeleo wa kanda hii, Magdi Shams El Din
ambaye ni mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya CAF na Rais wa Chama cha Mpira
wa Miguu Zanzibar (ZFA) ni miongoni mwa wageni watakaohudhuria mkutano
huo.
0 maoni:
Post a Comment