Monday, October 28, 2013

MCHEZAJI WA TIMU YA SAFARI POOL TAIFA, PATRICK NYANGUSI AMEIBUKA BINGWA WA AFRIKA KATIKA MASHINDANO YA MCHEZAJI MMOJA MMOJA(SINGLES)

Bingwa wa Afrika wa mchezo wa Pool kutoka Tanzania, Patrick Nyangusi (kushoto) akiwa na mpinzani wake, Vishen Jagdev kutoka Afrika Kusini kabla ya kuanza mchezo wa fainali uliofanyika jijini Blantyre nchini Malawi mwishoni mwa wiki.


Bingwa wa Afrika wa mchezo wa Pool kutoka Tanzania, Patrick Nyangusi akicheza dhidi ya mpinzani wake, Vishen Jagdev kutoka Afrika Kusini (hayupo pichani) wakati wa mchezo wa fainali uliofanyika Blantyre Malawi mwishoni mwa wiki.

Wachezaji na mashabiki wa timu ya Taifa ya Safari Pool ya nchini Tanzania wakiwa wamembeba mchezaji,Patrick Nyangusi mara baada ya kutwaa ubingwa wa Afrika wa mchezaji mmoja mmoja (Singles) kwa kumfunga Vishen Jagdev wa Afrika Kusini 6-4,katika mchezo uliofanyika Blantyre Malawi mwishoni mwa wiki.

Wachezaji na mashabiki wa timu ya Safari Pool kutoka Tanzania wakishandilia na mchezaji Patrick Nyangusi mara baada ya kutwaa ubingwa wa mchezaji mmoja mmoja (Singles) Afrika uliofanyika Blantyre Malawi mwishoni mwa wiki.

Wachezaji wa timu ya Taifa ya Safari Pool ya Tanzania wakiwa na medali zao za Fedha mara baada ya kutunukiwa kwa kupata nafasi ya tatu katika mashindano ya Pool Afrika yaliyofanyika jijini Blantyre Malawi mwishoni mwa wiki

Mgeni rasmi,Mjumbe wa Baraza la Michezo Nchini Malawi, Sharaf Pinto(wa pili kushoto) akiwa na mabingwa wa Singles(mchezaji mmoja mmoja).Kutoka kulia ni mshindi wa tatu kutoka Zambia, Moses Mofya,mshindi wa pili kutoka Afrika Kusini, Vishen Jagdev na Bingwa gwa Afrika kutoka Tanzania, Patrick Nyangusi wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kuwakabidhi medali zao Blantyre Malawi mwishoni mwa wiki.

Mabingwa wa Afrika  wa mchezo wa pool wakiwa katika picha nya pamoja.Kutoka kushoto ni Bingwa wa Afrika kutoka Tnzania, Patrick Nyangusi,mshindi wa pili kutoka Afrika Kusini, Vishen Jagdev na mshindi wa tatu kutoka Zambia, Moses Mofya mara baada ya kukabidhiwa zawadi zao jijini Blantyre Malawi mwishoni mwa wiki.

Bingwa wa Afrika wa Safari Pool kutoka Tanzania, Patrick Nyangusi akiwa katika picha ya pamoja na warembo wa Blantyre Malawi mara baada ya kukabidhiwa zawadi ya medali ya zahabu mwishoni mwa wiki.

0 maoni:

Post a Comment

WANAOTEMBELEA KWA SIKU