Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) kuwania ubingwa wa Tanzania Bara inakamilisha raundi
ya kumi na moja kesho (Oktoba 29 mwaka huu) kwa mechi tatu huku Yanga
ikiwa mwenyeji wa Mgambo Shooting kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Uwanja
wa Kumbukumbu ya Sokoine jijini Mbeya utakuwa mwenyeji wa mechi kati ya
Mbeya City na Tanzania Prisons. Rhino Rangers na JKT Ruvu zitacheza
katika Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi mjini Tabora.
Raundi
ya 12 ya ligi hiyo itaanza Oktoba 31 mwaka huu kwa mechi kati ya Simba
na Kagera Sugar kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam wakati Novemba
Mosi mwaka huu kutakuwa na mechi kati ya Yanga na JKT Ruvu kwenye uwanja
huo huo.
Novemba
2 mwaka huu kutakuwa na mechi nne; Mgambo Shooting na Coastal Union
(Uwanja wa Mkwakwani, Tanga), Tanzania Prisons na Oljoro JKT (Uwanja wa
Sokoine, Mbeya), Azam na Ruvu Shooting (Azam Complex, Dar es Salaam), na
Mtibwa Sugar na Rhino Rangers (Uwanja wa Manungu, Morogoro).
Raundi
hiyo itakamilika Novemba 3 mwaka huu kwa mechi moja ambapo Mbeya City
itakuwa mwenyeji wa Ashanti United kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya
Sokoine jijini Mbeya.
Mechi
za kukamilisha mzunguko wa kwanza wa ligi hiyo zitachezwa Novemba 6 na 7
mwaka huu. Novemba 6 ni JKT Ruvu vs Coastal Union, Ashani United vs
Simba, Kagera Sugar vs Mgambo Shooting, Rhino Rangers vs Tanzania
Prisons na Ruvu Shooting vs Mtibwa Sugar.
Novemba 7 mwaka huu, Azam itacheza na Mbeya City wakati Yanga itacheza na Oljoro JKT kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
EL MAAMRY KUONGOZA BODI YA TFF
Mkutano
Mkuu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) umemteua Said Hamad
El Maamry kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ambayo kazi yake kubwa
ni kusimamia mali za shirikisho.
El
Maamry ambaye kitaaluma ni mwanasheria na Mwenyekiti wa zamani wa TFF
wakati huo ikiwa Chama cha Mpira wa Miguu Tanzania (FAT) ataongoza bodi
hiyo yenye jumla ya wajumbe watano.
Wajumbe
wengine wa bodi hiyo ni Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Joel Bendera ambaye
anakuwa Makamu Mwenyekiti, Dk. Ramadhan Dau, Mohamed Abdulaziz na
aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Stephen Mashishanga.
0 maoni:
Post a Comment