MAMBO YANAENDELEA! Tamasha
la wanamitindo na wabunifu walio katika vyuo vikuu lijulikanalo kama ‘Redd’s
Uni-Fashion Bash’, mwishoni mwa wiki hii linatarajiwa kufanyika mkoani
Kilimanjaro, baada ya Mwanza kufungua pazia.
Tamasha hilo linalochochea
vipaji ndani ya vyuo hivyo, mbali na Mwanza na Kilimanjaro pia litahusisha vyuo
vilivyopo katika Mikoa ya Dar es Salaa na Iringa.
Akizungumzia tamasha hilo,
Meneja Masoko wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), Fimbo Butallah alisema,
linatarajiwa kufanyika Jumapili ndani ya ukumbi wa Glessius uliopo mjini hapa.
Fimbo alisema, wanafunzi
wa vyuo vyote vya elimu ya juu walio na mapenzi katika ubunifu na mitindo
wanatarajiwa kushiriki shindano hilo, huku akiamini kukiwa na upinzani mkali
zaidi ya ule wa Mwanza.
“Siku zote tunaamini
katika kukuza vipaji zaidi, ila siku hiyo kutakuwa na burudani kali kutoka kwa
msanii Jon Makini,” alisema Butallah.
Katika tamasha la awali
lililofanyika Mwanza, kulikuwa na ushindani mkali katika mitindo ambapo Fahad
Rajab kutoka Chuo Kikuu cha St. Augustine (SAUT) aliibuka mshindi akifuatiwa na
Lucy Charles kutoka pia chuo hicho.
Fahad kwa ushindi huo
alijinyakulia Sh 500,000 huku Lucy akitwaa Sh 400,000 na mshindi wa tatu Ally Thabit
wa Chuo cha Biashara (CBE) akiondoka na Sh 300,000 huku Joseph Mmari wa SAUT
aliyeshika nafasi ya nne pamoja na Victoria Newton pia kutoka chuo hicho
aliyeshika nafasi ya tani kila mmoja akipata Sh 100,000.
Kwa upande wa wabunifu
mshindi wa kwanza alikuwa Dotto Elius wa CBE aliyejitwalia Sh 700,000,
akifuatiwa na Fahad Rajab wa SAUT aliyepata Sh 500,000 akifuatiwa na Rafaka
Mtani wa Taasisisya Uhasibu (TIA) aliyeondoka na Sh 300,000.
Washindi wa nne na watano
walikuwa ni Amedias Amedia wa SAUT na Elizabeth Mtani wa TIA ambao kila mmoja
aliondoka na Sh 100,000.
Meneja Habari na
Mawasiliano wa TBL, Edith Mushi alisema katika tamasha la leo, kwa upande wa
wabunifu mshindi wa kwanza ataondoka na Sh 700,000 wa pili Sh 500,000 watatu Sh
300,000 huku wa nne na watano kila mmoja akiondoka na Sh 100,000.
“Tunataka kuinua vipaji
vya wanafunzi wa vyuo katika tasnia ya mitindo, kwa sasa wanafunzi katika mikoa
iliyobaki wanatakiwa wajiandae mno, maana kuna upinzani mkubwa,” alisema Edith.
Alisema, ana imani kubwa
watafanikiwa kuinua vipaji vya wanafunzi walio wanamitindo na wabunifu.
“Tuna imani kubwa zawadi
hizi pia zitaongeza chachu kwa wabunifu na wanamitindo kuendeleza fani hii ya
mitindo. Lakini matamasha haya pia yatahusisha burudani za aina mbalimbali za
kuvutia.
“Hii itakuwa sehemu muhimu
ya kuwakutanisha wanafunzi wa vyuo na kada mbalimbali katika kufurahia na
kubadilishana mawazo juu ya masuala ya ubunifu na mitindo, kwani kinywaji cha
Redd’s Original kimekuwa mstari wa mbele katika kuendeleza tasnia ya urembo,
ubunifu na mitindo hapa nchini,” alisema Edith.
Kinywaji cha Redd’s
Original pia ndicho kinachodhamini shindano la Redd’s Miss Tanzania na
kinazalishwa na kusambazwa na Kampuni ya Bia Tanzania (TBL).
0 maoni:
Post a Comment