Rais Kikwete
FOMU za mbio ndefu za
Uhuru, maarufu kama Uhuru Marathon, zinatarajiwa kuanza kuuzwa rasmi kuan zia
kesho, huku Rais Jakaya Kikwete akitarajiwa kuchukua fomu namba moja.
Akizungumza na waandishi
wa habari jijini Dar es Salaam jana, Katibu wa Kamati ya Uhuru Marathon,
Innocent Melleck alisema, Rais Kikwete ndiye atakayepewa fomu nambo moja kwa
ajili ya kushirikishi mbio hizo.
“Hizi mbio zina maana
kubwa mno ndani ya Taifa letu, Rais Jakaya Kikwete muda wote anasisitiza na
kupigania amani. Amani ni yetu sote, si vyema kumuachia Rais Kikwete peke yake
kuipigania, hivyo yeye ndiye atakayekuwa namba moja katika kuchukua fomu na
kushiriki mbio hizo,” alisema.
Melleck alisema, katika
kuhakikisha kila mtu anashiriki kutakuwa na vituo 13 vitakavyofunguliwa kwa
ajili ya kutoa fomu hizo, huku pia kukiwa na watu maalumu watakaozisambaza
maofisini na hata majumbani.
Melleck alisema, fomu hizo
zitatolewa kwa Sh 100,000 kwa wale watakaotaka kukimbia mbio za kilomita tatu,
Sh 2,000 mbio za kilomita tano, Sh 6,000 kwa atakayeshiriki moja kati yam bio
za kilomita 21 au 42.
“Hizi mbio ni muhimu zaidi
kwa ajili ya Taifa letu, hivyo ni vyema kwa Watanzania wote wakashiriki ili
kuipigania amani iliyopo nchini mwetu.
“Tunataka kuungana na Rais
Kikwete katika kuhakikisha tunakuwa sehemu ya kuleta umoja, amani na mshikamano
ndani ya Tanzania na ndilo lengu la mbio hizi.
“Bado tunaendelea kuwaomba
wadhamini wajitokeze kuzidhamini, kwani nafasi bado ipo wazi na watambue hata
wao ni sehemu ya kupigania amani ya taifa letu,” alisema Melleck.
Katika mbio hizo,
zitakazowashirikisha watu wa kada mbalimbali, zitakuwepo pia mbio za kilomita
3, kilomita 5, Half Marathon kilomita 21 pamoja na Full Marathon yenyewe
kilomita 42.
Mratibu huyo anasema mbio
za kilomita 3 zitakuwa maalumu kwa ajili ya viongozi wa kada mbalimbali,
wakiwemo pia wale wa dini na zile za kilomita 5 pia zitakuwa za kuchangia kwa
ajili ya watu wa mahitaji ya aina mbalimbali.
“Hapa tunachotaka kufanya
katika mbio za kilomita 3 ni kuwaomba kama vile viongozi maarufu wa dini
mbalimbali pamoja na viongozi wetu ili kushiriki, kwa kudumisha amani na
upendo.
“Pia tutahakikisha kama
mbio za kilomita 5, zinakuwa kwa ajili ya kuchangia watu wenye mahitaji
mbalimbali na tayari tuna uhakika mkubwa wa wanariadha maarufu zaidi duniani
kushiriki,” Alisema.
Melleck alisema, wamejipanga
mno ili kuhakikisha wanafanya mambo makubwa zaidi na ambayo yataleta tija kwa
taifa.
0 maoni:
Post a Comment